Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Adabu ya ndoa

Katika somo hili, tutajifunza kuhusu adabu kadhaa za ndoa.

  • Kubainisha umuhimu wa kila mmoja wa wanandoa wapya kuwa na adabu za ndoa.
  • Kujua idadi kadhaa ya adabu muhimu zaidi za ndoa ambazo Uislamu ulielekeza kuwa nazo.

Mbali na hukumu za kisheria zinazohusiana na ndoa, ambazo baadhi yake huwa kabla ya mkataba wa ndoa, na baadhi yake huwa wakati wa mkataba, na baadhi yake huwa baada yake, Uislamu umeizunguka ndoa kwa mkusanyiko wa adabu ambazo kila mmoja wa wanandoa anapaswa kudumisha; ili kupata thawabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kwa matumaini ya kuhifadhi nguvu na uimara wa uhusiano wa kindoa.

1. Nia

Niya ina nafasi kubwa katika Uislamu, kama inavyothibitishwa na hadithi hii maarufu, "Hakika matendo yanategemea niya tu, na hakika kila mtu atapata kile alichokusudia." (Al-Bukhari 1, na Muslim 1907) Kwa hivyo wanandoa wanapaswa kuwa na niya njema katika ndoa. Bali katika ufahamu mzuri ni kwamba wazidishe niya nzuri ili wazidishe thawabu zao. Na katika niya njema katika ndoa ni kuonyesha moja ya ishara za Mwenyezi Mungu, kufuata amri za kisheria zinazotakwa katika ndoa, kutumaini kwamba uzao mzuri utaibuka kutoka kwao ambao watampwekesha na kumuabudu Mwenyezi Mungu, kila mmoja wa wanandoa kumuweka safi mwenzake na kumlinda kutokana na majaribio, na mambo mengineyo.

2- Kufuata Sunna katika usiku wa kukutana kwa wanandoa

١
Mume anafaa kumfanyia mkewe upole wakati wa kukutana naye mara ya kwanza.
٢
Mume anafaa kuuweka mkono wake kwenye nywele za mbele ya kichwa cha mke wake na aombe dua ambayo Nabii - rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, - alitufundisha, "Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba katika heri yake na katika heri ya kile kilichowekwa ndani yake. Na ninajikinga kwako kutokana na shari yake na shari ya kile kilichowekwa ndani yake." (Ibn Majah 1918)
٣
Mume kuswali rakaa mbili pamoja na mkewe, kama walivyoelekeza hivyo baadhi ya maswahaba.
٤
Kuomba dua kabla ya tendo la ndoa, aseme, "Kwa jina la Mwenyezi Mungu, ewe Mwenyezi Mungu, tuweke mbali na shetani, na ukiweke mbali na shetani utakachoturuzuku." (Al-Bukhari 3271, Muslim 1434). Na ni sawa kama mwanamke pia atasema hivyo.
٥
Kuepuka yale ambayo Mwenyezi Mungu Mtukufu ameharamisha wakati wa tendo la ndoa, ambapo ni haramu kwa mwanamume kumuingilia mkewe katika tupu ya nyuma au wakati wa hedhi.
٦
Ikiwa mwanamume atafanya tendo la ndoa na mke wake kisha akataka kurudia, basi ni sunna kwake kutawadha, kwa mujibu wa hadithi: “Ikiwa mmoja wenu atamjia mkewe, kisha akataka kurudia, basi na atawadhe.” (Muslim 308)
٧
Mume au mke kutoeneza siri za kujamiiana kwao. Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alisema, “Hakika, miongoni mwa watu waovu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu katika cheo Siku ya Kiyama, ni mwanamume anayemuingilia mkewe, naye mkewe akamuingilia, kisha akaeneza siri zake.” (Muslim 1437)

3- Karamu ya ndoa

Karamu ya ndoa ni sunna iliyosisitizwa, kwa mujibu wa kauli yake Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, akimwambia ʻAbdur-Rahman bin ʻAwf, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, alipooa, “Fanya karamu walau kwa kondoo mmoja.” (Al-Bukhari 2048, Muslim 1427)

Kinachopasa kuzingatiwa kwenye karamu

١
Asiwaalike matajiri peke yao, kwa mujibu wa kauli yake Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, "Chakula kiovu mno ni chakula cha karamu ambacho matajiri tu ndio wanaalikwa na maskini wanaachwa." (Al-Bukhari 5177, Muslim 1432)
٢
Karamu iwe kwa kondoo mmoja au zaidi ikiwa kuna uwezo, lakini bila ya kupitiliza kiasi.
٣
Inaruhusika kwamba karamu iwe bila nyama.

4- Wanawake kuimba kwenye harusi

Inaruhusiwa kwa wanawake tu kuimba kwa maneno mazuri ambayo yanaruhusiwa na kupiga ngoma huku wakiwa mbali na wanaume, na bila ya kutumia vyombo vya muziki. Kwa maana, kuonyesha furaha katika hafla hii nzuri inaruhusiwa katika Uislamu.

5. Kuishi pamoja kwa wema

Miongoni mwa adabu za ndoa zinazosisitizwa ni kuishi pamoja kwa wema; ili udumu upendo, ambao wanandoa hao wataishi kwa huo maisha ya furaha, Mwenyezi Mungu Mtukufu akipenda. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu, "Na kaeni nao kwa wema." (An-Nisaa: 19)

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani