Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Mapato machafu na miamala inayohusiana na mali iliyoharamishwa

Katika somo hili, tutajifunza kuhusu maana ya mapato machafu, sababu zake na madhara yake, na pia kujifunza kuhusu maana ya miamala inayohusiana na mali iliyoharamishwa.

  • Kujifunza kuhusu mapato machafu na kubainisha madhara yake.
  • Kujifunza kuhusu miamala inayohusiana na mali iliyoharamishwa.

Kuna kuchuma ambako ni kuzuri na halali, lakini pia kuna kuchuma ambako ni kuchafu na haramu. Mwenyezi Mungu amesema: "Enyi mlioamini! Toeni katika vile vizuri mlivyovichuma, na katika vile tulivyokutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya." [Al-Baqarah: 267]

Katika Hadith ya Abu Huraira, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, alisema: "Hakika zama zitawajia watu ambapo mtu hatajali ni wapi anapata (anachuma) mali yake; je, ni kwa njia ya halali au ya haramu?" (Al-Bukhari 2083)

Mapato machafu

Ni kula mali za watu kwa batili, au kuchuma kupitia njia ambayo imeharamishwa na Sheria.

Njia mbaya za kuchuma mali

١
Hili huwa kwa njia ya kula mali za watu kwa batili, kama vile kuchukua mali za wengine kwa njia ya dhuluma, ulaghai, udanganyifu, au unyang'anyi, au bila ya ridha ya mmiliki wake.
٢
Pia huwa kwa njia ya miamala ilyoharamishwa kisheria, kama vile riba, kamari, na uuzaji wa vitu vilivyoharamishwa, kama vile divai, nyama ya nguruwe, vyombo vya muziki na mengineyo.

Sababu za kujihusisha na mapato mabaya

١
Kutomhofu na kumstahi Mwenyezi Mungu. Hii ni kwa sababu hofu na staha kwa Mwenyezi Mungu vinapoondolewa moyoni mwa mtu, basi yeye hajali kama mapato yake ni ya halali au ni ya haramu.
٢
Kuwania kupata mali haraka: Watu wengine hawana uvumilivu, na wanataka kupata mali nyingi kwa muda mfupi zaidi, jambo ambalo huwasukuma kula haramu.
٣
Tamaa na kutotosheka: Watu wengine hawaridhii na kile ambacho Mwenyezi Mungu amewagawia katika riziki ya halali. Kwa hivyo wanafanya juhudi kutafuta zaidi, hata ikiwa ni kile ambacho Mwenyezi Mungu aliharamisha.

Madhara ya mapato mabaya

١
Kupatwa na hasira ya Mwenye kufanya atakalo na kuingia Motoni. Imesimuliwa kutoka kwa Abu Umama, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kuwa alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema: "Yeyote atakayechukua haki ya mtu Mwislamu kwa kiapo chake (cha uongo), basi kwa hakika, Mwenyezi Mungu ameshamuwajibishia kuingia Motoni na akamharamishia Pepo." Mwanamume mmoja akasema, "Hata kama ni kitu kidogo tu, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu." Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, akasema, "(Ndiyo) hata kama ni kijiti cha (mti wa) Arak.” (Muslim 137)
٢
Giza la moyo, uvivu wa viungo katika kumtii Mola Mlezi, aliyetakasika, kuondoa baraka katika riziki na umri wa mtu.
٣
Kutokubaliwa dua. Imesimuliwa kutoka kwa Abu Huraira, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kwamba: Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alimtaja mwanamume mmoja aliyekuwa katika safari ndefu, hali ya kuwa ametimka nywele, ana mavumbi. Akawa ananyoosha mikono yake mbinguni (kuomba dua), 'Ewe Mola Mlezi, ewe Mola Mlezi;' ilhali chakula chake ni haramu, kinywaji chake ni haramu, nguo yake ni haramu, na alilishwa vya haramu. Basi vipi ataitikiwa dua yake?" (Muslim 1015)
٤
Kutokea uadui na chuki kati ya watu na kutengana kwa jamii. Haya ndiyo matokeo yasiyoepukika yanayotokana na kuvunja mipaka kuhusiana na mali za watu na kuzila kwa batili. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema, "Hakika Shetani anataka kutia kati yenu uadui na chuki kwa ulevi na kamari..." [Surat Maida: 91]

Aina za vitu vilivyoharamishwa katika Miamala inayohusiana na mali

١
Vitu vyenyewe vilivyoharamishwa
٢
Vitendo vilivyoharamishwa

Vitu vyenyewe vilivyoharamishwa

Ni kila kitu kilichoharamishwa chenyewe, kama vile nyamafu, damu, nyama ya nguruwe, vitu vichafu na najisi na vinginevyo. Hivyo ni miongoni mwa mambo ambayo nafsi yenyewe haivipendi. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Sema: Sioni katika yale niliyofunuliwa mimi kitu kilichoharamishwa kwa mlaji kukila isipokuwa kiwe ni nyamafu, au damu inayomwagika, au nyama ya nguruwe, kwani hiyo ni uchafu; au kwa upotofu kimechinjwa kwa jina la asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Lakini mwenye kushikwa na dharura, bila ya kutamani wala kuvuka mipaka, basi hakika Mola wako Mlezi ni Mwenye kusamehe, Mwingi wa kurehemu." [Al-An'am: 145]

Vitendo vilivyoharamishwa

Ni kila shughuli inayokiuka Sheria, kama vile riba, kamari, bahati nasibu, ulaghai, udanganyifu, kuhodhi mali na mengineyo ambayo yanajumuisha kuwadhulumu waja, na kula mali za watu kwa batili. Aina hii ndiyo ambayo inatamaniwa sana na nafsi. Ndiyo maana ilihitaji kukemewa na kuiwekea adhabu ambayo inazuia kujiingiza ndani yake. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Hakika wale wanaokula mali ya mayatima kwa dhuluma, hapana shaka yoyote wanakula matumboni mwao moto, na wataingia katika Moto wenye mwako mkali." Na Mwenyezi Mungu Mtukufu akasema: "Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na acheni riba zilizobakia, ikiwa nyinyi ni Waumini. Basi msipofanya, jitangazieni vita na Mwenyezi Mungu na Mtume wake." [Al-Baqarah: 278, 279]

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani