Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Mauzo

Katika somo hili, tutajifunza juu ya maana ya mauzo, na baadhi ya hukumu zake katika sheria ya Kiislamu.

  • Kujua hukumu ya mauzo.
  • Kujua hekima iliyoko nyuma ya kuhalalisha mauzo.
  • Kujua masharti ya mauzo.
  • Kuelezea misingi ya mauzo yaliyokatazwa ili kuyaepuka.

Maana ya Mauzo

Kuuza katika lugha ya Kiarabu kunamaanisha kubadilishana kitu kwa kitu. Na katika istilahi ya kisheria ni kubadilishana mali kwa mali kwa njia ya kumilikisha na kumiliki.

Hukumu ya mauzo

Kuuza na kununua ni mkataba unaoruhusiwa; kwa Kitabu, Sunna na maafikiano ya wanazuoni. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema, "Na Mwenyezi Mungu ameihalalisha biashara." [Al-Baqarah: 275]

Hekima ya kuruhusu mauzo

1- Mwanadamu anahitaji kile ambacho wengine wanakimiliki kama vile chakula, kinywaji, mavazi, makazi na mengineyo. Mmiliki wa vitu hivi hawezi kuvitoa bila malipo. Katika mauzo kuna njia ya mtu kufikia kile anachotaka; muuzaji apate thamani, naye mnunuzi apate bidhaa.

2- Kuendelea kwa maisha ya watu kwa njia bora zaidi; kwa sababu mwanadamu hawezi kukidhi mahitaji yake isipokuwa kwa kununua.

3. Kuzuia wizi, unyang'anyi, ulaghai na mambo mengine ambayo yanaharibu jamii, kwa sababu mwanadamu anaweza kupata mahitaji yake kwa kununua.

Nguzo za Mauzo:

١
Muuzaji: Naye ni mmiliki wa bidhaa.
٢
Mnunuzi: Naye ni mmiliki wa thamani ya bidhaa.
٣
Mbinu: Ni muuzaji kuwasilisha bidhaa, na mnunuzi kuikubali. Hayo yanatimia kwa kila chenye kuonyesha hayo miongoni mwa njia ambazo watu wanaona kuwa ni mauzo.
٤
Kinachofungiwa mkataba: Nacho ni thamani ya bidhaa na bidhaa yenyewe.

Masharti ya wana mkataba

١
Akili timamu: Kwa hivyo haiwi sahihi kuuza au kununua kwa mwendawazimu au mlevi.
٢
Kubalehe: Kunaruhusiwa kuuza kwa mtoto mdogo mwenye upambanuzi wa mambo, na asiyekuwa na upambanuzi katika vitu rahisi. Ama visivyokuwa rahisi, basi kunaruhusiwa kuuza au kununua kwa mtoto mdogo mwenye upambanuzi ikiwa mlezi wake atamuidhinisha. Ama asiyekuwa na upambanuzi, huyo kuuza au kununua kwake hakuruhusiwi.
٣
Kuwa na ruhusa ya kujitendea mambo: Kwa hivyo, hakuruhusiwi kuuza au kununua kwa yule aliyezuiliwa kwa sababu ya kutokuwa na uwezo wa kuendesha mambo sawasawa.
٤
Ridhaa na hiari: Hakuwi sawa kuuza au kununua kwa yule aliyelazimishwa bila haki, wala kuuza na kununua kwa afanyaye mchezo tu, wala kuuza na kununua kwa aliyelazimika, kama vile wana mkataba wawili kujionyesha kwamba wanauziana kwa sababu ya hofu juu ya mtu dhalimu ilhali hawana makusudio ya kuuza kiuhakika.
٥
Uwezo wa muuzaji kumkabidhi mnunuzi bidhaa: Na ikiwa hawezi, basi mauziano hayo hayawi sahihi.

Masharti ya kinachofanyiwa mkataba wa mauziano (thamani na bidhaa)

١
Kutofautisha kati ya bei (thamani) na bidhaa: Kwa maana mauziano yanaweza kuwa bidhaa kwa bidhaa, au bidhaa kwa pesa, au pesa kwa pesa. Kwa hivyo ni sharti kutofautisha kati yake.
٢
Kuwepo bidhaa: Hairuhusiwi kuuza kisichokuwepo wakati wa kufunga mkataba.
٣
Uhalali wa kile kinachouzwa: Hairuhusiwi kuuza mvinyo, nyama ya nguruwe, vyombo vya muziki na mambo mingineyo yaliyoharamishwa.
٤
Usafi wa mali inayouzwa: Hairuhusiwi kuuza mali iliyo najisi, wala kile kisichowezekana kusafishwa kutokana na najisi.
٥
Uwezo wa kuifikia bidhaa: Hairuhusiwi kuuza ndege aliye angani, wala gari lililoibiwa na mfano wa hayo.
٦
Kuwa na umiliki wa bidhaa: Hairuhusiwi kwa muuzaji kuuza kile ambacho hakimiliki, isipokuwa kama ameidhinishwa kukiuza.

Mauzo yaliyokatazwa

١
Haya ni mauzo yanayohusisha gharar, ambayo ni mauzo yanayohusisha hatari kwa mmoja wa wahusika wa mkataba, na yanasababisha mali yake kupotea, kama vile kuuza kitu kisichojulikana kuwepo kwake au kutokuwepo kwake, au kitu ambacho hakijulikani uchache wake na wingi wake, au haiwezekani kukikabidhi kwa mnunuzi.
٢
Mauzo yanayohusisha hadaa na madhara
٣
Mauzo yanayohusisha riba
٤
Kuuza kile ambacho kimeharamishwa kukiuza chenyewe, kama vile mnyama mfu, pombe na nguruwe.
٥
Mauzo yaliyoharamishwa kwa sababu ya kitu kingine, kama vile kuuza wakati wa wito wa pili siku ya Ijumaa, na kuuza kitu kinachokusudiwa kutengeneza kitu haramu, kama vile zabibu kwa ajili ya kutengeza pombe, na upanga kwa yule anayetaka kuua.

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani