Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Hadathi kubwa na kuoga

Uislamu uliweka sheria ya kuoga kwa ajili ya usafi kutokana na hadathi kubwa. Katika somo hili, utajifunza kuhusu sababu zinazomlazimu mtu kuoga na jinsi ya kujisafisha kutokana na hadathi kubwa.

  • Kujua sababu zinazomlazimu mtu kuoga.
  • Kujua jinsi ya kujisafisha kutokana na hadathi kubwa.

Sababu zinazomlazimu mtu kuoga

Ni mambo ambayo yakimtokea Muislamu, atasifika kwamba ana hadathi (uchafu) kubwa, na itamlazimu kuoga kabla ya kuswali na kufanya Tawaaf (kuzunguka kando ya Al-Kaba).

1. Kutoka manii

Kutoka manii kwa mtiririko kwa raha kwa njia yoyote ile, na katika kila hali, katika hali ya mtu kuwa macho au katika hali ya kulala. Na manii ni kioevu kinene cheupe ambacho hutoka wakati wa kilele cha matamanio ya kijinsia na raha.

2. Kufanya ngono

Kinachomaanishwa na tendo la ndoa ni kuingiza uume wa mwanaume ndani ya uke wa mwanamke, hata kama manii hayakutoka. Na inatosha kufanya kumlazimu mtu kuoga kwa kuingiza kichwa cha uume tu katika uke wa mwanamke.

3. Kutokwa damu ya hedhi na nifasi

Hedhi ni damu ya kawaida ambayo inamtoka mwanamke kila mwezi, na inaendelea kwa siku saba. Mara huzidi au kupungua kulingana na maumbile ya mwanamke. Nayo nifasi ni damu inayomtoka mwanamke kwa sababu ya kuzaa, na inaendelea kutoka kwa siku kadhaa.

Swala na saumu za wanawake wenye hedhi na wanawake walio katika nifasi

Haiwalazimu wanawake wenye hedhi na wale walio katika nifasi kuswali na kufunga saumu muda wa kutokwa na damu. Watalazimika kulipa saumu baada ya kusafika, lakini hawalazimiki kulipa swala.

Kujamiiana na wanawake walio katika hedhi na nifasi

Hairuhusiki kwa wanaume kuingiliana na wake zao wakati wa hedhi au baada ya kuzaa, lakini inaruhusika kustarehe nao bila ya kujamiiana nao. Wanatakiwa kuoga pindi damu inapokatika. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Basi jitengeni na wanawake wakati wa hedhi. Wala msiwaingilie mpaka watahirike. Wakishatahirika basi waendeeni alivyokuamrisheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wanaotubu na huwapenda wanaojisafisha." (Al-Baqara: 222) Na maana ya kauli yake, "Wakishatahirika," ni wakishaoga.

Muislamu anajisafisha vipi kutokana na janaba au hadathi kubwa?

Inamtosha Muislamu kukusudia kujisafisha na kuosha mwili wake wote kwa maji.

Jinsi alivyokuwa akioga Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Njia kamili zaidi ya kuoga ni kuoga kama alivyooga Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake. Kwa hivyo, Mwislamu anapotaka kuoga kutokana na janaba, ataosha viganja vyake, kisha aoshe sehemu zake za siri na uchafu wowote uliomuendea kutokana na janaba. Kisha atatawadha wudhuu kamili, kisha ataosha kichwa chake kwa maji mara tatu, kisha ataosha mwili wake wote.

Je, kuoga kunatosheleza kutawadha?

Muislamu akioga kwa sababu ya janaba, hilo linamtosha na hahitaji kutawadha. Bali lililo bora zaidi ni kutawadha kisha aoge, kama ilivyo katika Sunna ya Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani