Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Haki za wazazi

Katika somo hili, tutajifunza kuhusu maana ya kuwafanyia wema wazazi na baadhi ya yale yanayohusiana na hilo.

  • Kubainisha cheo kikubwa cha wazazi katika Uislamu.
  • Kuhimiza juu ya haki ya wazazi, na kutahadharisha dhidi ya kutowatii.
  • Kujua majukumu muhimu zaidi ya watoto kwa wazazi wao.
  • Kubainisha baadhi ya maadili katika kuamiliana na wazazi.

Cheo cha wazazi katika Uislamu

Uislamu uliwaheshimu wazazi kwa heshima kubwa, na ukaunganisha kuwafanyia wema na amri kubwa zaidi katika Uislamu, ambayo ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu Mtukufu. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema, "Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote isipokuwa Yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema." [Al-Israa: 23] Mwenyezi Mungu Mtukufu amewafanya wazazi kuwa sababu ya kuwepo kwa wana wa kiume na mabinti, na hata wana wakifanya watakachofanya ili kurudisha chochote katika wema wao juu yao, kamwe hawataweza kurudisha chochote katika wema huo wa wazazi wao juu yao, wala kuwalipa kwa taabu, uchovu, madhara, kukesha, na ukosefu wa raha waliopata kwa ajili ya furaha ya watoto wao, ili kuwatunza na kuwalinda.

Katika uadilifu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kwamba aliwapa wazazi haki juu ya wana wao, ziwe malipo kwao kwa sababu ya juhudi nzuri ambazo walifanya kwa wingi katika kuwatunza. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema, "Na tumemuusia mwanadamu awatendee wema wazazi wake wawili." [Ankabut: 8] Na akasema, "Lakini kaa nao kwa wema duniani." [Luqman: 15] Na wakati mmoja wa maswahaba alipomuuliza Mtume - rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, - 'Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, ni nani anayestahiki zaidi nikae vyema naye?' Akasema, "Mama yako." Akasema, 'Kisha nani?' Akasema, "Kisha mama yako." Akasema, 'Kisha nani?' Akasema, "Kisha mama yako." Akasema, 'Kisha nani?' Akasema, “Kisha baba yako.” (Al-Bukhari 5971, Muslim 2548)

Fadhila ya kuwafanyia wema wazazi

Kuwafanyia wema wazazi ni wajibu kwa watoto, na katika kuwafanyia wema kuna malipo makubwa, na ni sababu ya kubarikiwa na kuruzukiwa, na kupata heri nyingi katika dunia hii, na ni sababu ya kuingia Peponi huko Akhera. Nabii - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie - alisema, "Limeangamia pua lake, kisha limeangamia pua lake, kisha limeangamia pua lake." Ikasemwa: Ni nani huyo ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema, "Ni yule aliyewapata wazazi wake katika uzee, mmoja wao, au wote wawili, kisha asiingie Peponi." (Muslim 2551)

Kuwafanyia wema wazazi ni mojawapo ya matendo bora zaidi na ambalo ni pendwa zaidi kwa Mwenyezi Mungu. Abdullah bin Masud, Mwenyezi Mungu amridhie, alimuuliza Nabii - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, - 'Ni kazi gani inayopendwa zaidi na Mwenyezi Mungu?' Akasema, "Swala kwa wakati wake." Akasema, 'Halafu nini?' Akasema, "Halafu kuwafanyia wema wazazi." Akasema, 'Halafu nini? 'Akasema, “Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu.” (Al-Bukhari 527, Muslim 85)

Kwa hivyo, kuwafanyia wema wazazi ni bora kuliko jihadi ya sunna. Mwanamume mmoja alimjia Nabii - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie - na akasema, 'Niende katika Jihadi?' Akasema, "Una wazazi?" Akasema, 'Ndiyo.' Akasema, "Basi fanya jihadi katika hao." (Al-Bukhari 5972, Muslim 2549)

Kuwatotii wazazi

Kutotii wazazi ni moja ya dhambi kubwa zaidi. Katika hadithi, Nabii - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie - alisema, "Madhambi makubwa zaidi ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu, na kuwaasi wazazi..." hadi mwisho wa hadithi. (Al-Bukhari 6919, Muslim 87)

Wajibu wa watoto kwa wazazi

١
Kuwatii kwa kile wanachoamrisha ya wema maadamu amri hizo ziko ndani ya mipaka ya uwezo wao. Lakini ikiwa wataamrisha maasia, basi asiwatii katika hilo, kwa maana hakuna utii kwa kiumbe katika kumuasi Muumba.
٢
Kukaa nao kwa wema, hata kama watamkosea mwana. Na je kuna kosa lolote kubwa zaidi kuliko wao kumwita kwenye ushirikina na kukaa milele Motoni? Na pamoja na hivyo, Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema, "Na pindi wakipambana nawe ili unishirikishe na ambayo huna elimu nayo, basi usiwatii. Lakini kaa nao kwa wema duniani." [Luqman: 15]
٣
Kuwajali na kuwafanyia wema, na hilo ni kwa kuwafanyia kila aina ya wema, huduma na utii, pamoja na kuwapenda na kuamiliana nao kwa maadili na adabu bora zaidi. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema, "Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema." [Al-Israa: 23]
٤
Kutowadhuru au kuwafanyia ubaya hata kwa aina yake ndogo zaidi, hata kwa neno "Ah!", haswa ikiwa ni wazee. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema, "Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata, 'Ah!' Wala usiwakemee. Na sema nao kwa maneno ya heshima." [Al-Israa: 23]
٥
Kuwashushia bawa na kujiweka chini mbele yao, kama Mwenyezi Mungu Mtukufu alivyosema, "Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma. Na useme: Mola wangu Mlezi! Warehemu kama walivyonilea utotoni." [Al-Israa: 24]
٦
Kudumu katika kuwashukuru na kutambua fadhila zao. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema, "Na tumemuusia mtu kwa wazazi wake wawili. Mama yake ameibeba mimba yake kwa udhaifu juu ya udhaifu, na kumwachisha ziwa baada ya miaka miwili. (Tumemuusia): Nishukuru Mimi na wazazi wako. Ni kwangu Mimi ndiyo marudio yenu." [Luqman: 14]
٧
Nabii - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie - alisema, “Wewe na mali yako ni wa baba yako. Hakika wana wenu ni katika vizuri zaidi mlivyochuma. Basi kuleni katika vile walivyochuma wana wenu.” (Abu Dawud 3530)
٨
Kuwaombea dua katika maisha yao na baada ya kufa kwao. Mtume wa Mwenyezi Mungu - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie -alisema, "Mtu anapokufa, matendo yake hukatika isipokuwa kwa mambo matatu: isipokuwa sadaka inayoendelea, au elimu yenye kuwanufaisha wengine, au mwana mwema anayemuombea." (Muslim, 1631)
٩
Kuwakirimu marafiki wa wazazi baada ya kifo chao. Nabii - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie - alisema, “Hakika, wema kwa wazazi ulio mkubwa zaidi ni mwana kuwaunga watu aliokuwa baba yake akiwapenda.” (Muslim 2552)

Maadili ambayo ni ya lazima katika kuamiliana na wazazi

١
Kuwasikiliza vizuri katika mazungumzo yao na kutojishughulisha mbali nao na chochote, kama vile simu na mengineyo.
٢
Kuharakisha kufanya kile wanachopenda kabla ya kukiomba, na kuwaondolea kila chenye kuwasumbua kabla hakijawajia.
٣
Kuwaitikia haraka pamoja na kuonyesha ridhaa katika kuitikia huko na kutochelewa.
٤
Kuwanasihi kwa ulaini na hekima endapo mzazi ataanguka katika maasia.
٥
Kukabiliana na ukatili na dhuluma ya wazazi - ikiwa hayo yatatokea - kwa uvumilivu, wema na heshima.
٦
Kutokuwa mkaidi na kuwapa changamoto.
٧
Kutabasamu sana mbele yao.
٨
Kuwashauri, kuwashirikisha katika mambo ya mtu binafsi, na kuheshimu maoni yao.
٩
Kufanya bidii katika kuzungumza nao na kuwa wazi mbele yao, hata katika masuala ya kila siku ya maisha ikiwa wanapenda hivyo.
١٠
Katika hali ya kutengana kwa sababu ya safari, mwana anapaswa kuwasiliana naye kila wakati na kuhakikisha wako katika hali nzuri.

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani