Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Kufunga saumu kwa hiari

Mwenyezi Mungu amefaradhisha kufunga saumu ya mwezi mmoja katika mwaka, lakini pia alihimiza kufunga katika siku nyinginezo ili kutafuta malipo zaidi. Katika somo hili, utajifunza kuhusu aina kadhaa za funga za kujitolea na fadhila zake.

  • Kujifunza baadhi ya aina za funga za kujitolea.
  • Kujua fadhila na thawabu za aina hizi za funga.

Mwenyezi Mungu alilazimisha kufunga saumu mwezi mmoja katika mwaka, lakini alihimiza kufunga saumu katika siku nyinginezo kwa mwenye uwezo na hamu ya kufanya hivyo ili kutafuta malipo zaidi, na miongoni mwa siku hizo ni:

1. Siku ya Ashura

Ni siku ya kumi ya mwezi wa Muharram; mwezi wa kwanza katika kalenda ya Kiislamu. Hii ni siku ambayo Mwenyezi Mungu alimwokoa Nabii wake Musa, amani iwe juu yake, kutoka kwa Firauni. Kwa hivyo Muislamu anaifunga ili kumshukuru Mwenyezi Mungu juu ya kumuokoa Musa, amani iwe juu yake, na kumfuata Mtume wetu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, kwa sababu aliifunga. Alipoulizwa juu ya kufunga saumu siku ya Ashura, alisema: "Inasamehe dhambi za mwaka uliopita." (Muslim 1162). Inapendekezwa kufunga saumu siku moja kabla yake, siku ya tisa. Imesimuliwa kutoka kwa Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, kwamba alisema: "Ikiwa nitabakia mpaka mwaka ujao, basi hakika nitafunga saumu siku ya tisa." (Muslim 1134)

2. Siku ya Arafa

Ni siku ya tisa ya mwezi wa Dhul-Hijja, mwezi wa kumi na mbili wa kalenda ya Kiislamu. Siku hii ni wakati ambapo mahujaji waliohiji Nyumba ya Mwenyezi Mungu hukusanyika Arafa na kumuomba Mwenyezi Mungu, na ndiyo siku bora ya mwaka. Anaruhusiwa kufunga siku hii mtu asiyekuwa hujaji. Mtume rehema na amani ziwe juu yake, alipoulizwa juu ya kufunga siku ya Arafa, alisema: "Ni kafara ya madhambi ya mwaka uliopita na mwaka uliopo." (Muslim 1162)

3. Siku sita katika mwezi wa Shawwal

Shawwal ni mwezi wa kumi wa kalenda ya Kiislamu. Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alisema: "Atakayefunga Ramadhani kisha akaifuatisha siku sita katika mwezi wa Shawwal, huwa ni kama amefunga mwaka mzima." (Muslim 1164)

4. Kufunga siku tatu katika kila mwezi

Imesimuliwa kutoka kwa Abu Huraira, Mwenyezi Mungu amridhie, kuwa alisema: "Rafiki yangu mwandani aliniusia mambo matatu ambayo sitaacha mpaka nitakapokufa: kufunga siku tatu katika kila mwezi, swala ya dhuha, na kulala hali ya kuwa nimeswali witri." (Al-Bukhari 1178, Muslim 721)

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani