Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Safari na usafi

Kuna hali mbalimbali zinazohusiana na usafi ambazo Muislamu hukabiliwa nazo anapokuwa safarini.

  • Kujifunza kuhusu hukumu za usafi kwenye safari.

Katika safari, mengi katika yale ambayo mtu alikuwa akiyakuta katika makazi yake nyumbani na vitu vilivyo karibu naye hubadilika. Imesimuliwa kutoka kwa Abu Huraira, Mwenyezi Mungu amridhie, kutoka kwa Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kwamba alisema: "Safari ni aina ya adhabu kwa kuwa inamzuia mmoja wenu kula, kunywa na kulala vizuri. Hivyo basi, pindi mtu atakapomaliza mahitaji yake, basi na aharakishe kurejea kwa familia yake." (Al-Bukhari 1804, 3001, 5429, na Muslim 1927) Kwa hivyo, inampasa mtu anayekwenda safarini kujua mambo kadhaa miongoni mwa masuala ya usafi na mengineyo, ikiwa ni pamoja na:

1. Kuchagua mahali pazuri pa kukidhi haja ya asili

Ni haramu kukidhia haja ya asili katika maeneo yanayotembelewa mara kwa mara na watu kama vile kivuli, miti, au eneo ambalo limeandaliwa kwa ajili ya kukaa hapo.

Wanazuoni walisema kwamba ikiwa alikuwa jangwani na mfano wake, na akataka kukidhi haja ya asili, basi inapendekezwa kwamba atafute mahali laini; ili asalimike kutokana na kujichafua na mkojo, na ili pia mkojo wake usimrukie. Basi asikidhie haja yake katika mahali pagumu, na vile vile asielekee upande ambapo upepo unatokea.

2. Kujisitiri wakati wa kukidhi haja ya asili

Ni lazima kujisitiri mbali na watu mtu anapokidhi haja ya asili, ima kwa kizuizi au kwenda mbali na watu, kwa mujibu wa hadithi ya Al-Mughirah bin Shu'ba, kuwa alisema: "Nilikuwa pamoja na Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, katika safari na akasema, 'Ewe Mughira! Chukua chombo hiki cha maji.' Nilikitwaa, na Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, akaenda mbali hata alipopotea nikashindwa kumuona, kisha akakidhi haja yake ya asili." (Al-Bukhari 363, na Muslim 274) Katika hadithi nyingine: “Alikuwa anapofika mahali pa kukidhi haja yake ya asili, anahakikisha amekwenda mbali zaidi." (Musnad Imam Ahmad 15660)

Na katika Hadithi ya Abdullah bin Ja'far, ambamo alimtaja Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: “Na kilikuwa kitu anachopenda zaidi Mtume wa Mwenyezi Mungu,rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kujisitiri kwacho wakati wa kukidhi haja yake ya asili ni mahali pa mwinuko (kama vile kilima) au mkusanyiko wa mitende." (Muslim 342) Na ilikuja katika Hadithi nyingine kwamba, “Alikuwa anapotaka kukidhi haja yake ya asili, hangeinua vazi lake mpaka awe karibu zaidi na ardhi." (Abu Dawud 14), kwa sababu hilo linasitiri zaidi.

Tayammam:

Tayammam ni aina ya usafi kwa ajili ya swala wakati hakuna maji au ikiwa mtu hawezi kuyatumia. Hilo huwa kwamba Muislamu apige vumbi la ardhi kwa viganja vyake, kisha afute kwavyo uso wake, kisha akifute kwavyo kiganja chake cha kulia kwa kiganja chake cha kushoto, kisha afute kwavyo kiganja chake cha kushoto kwa kiganja chake cha kulia.

Muislamu anahitaji kufanya tayammam zaidi kwenye safari kuliko anapokuwa hayuko safarini, kwa sababu nyingi ambazo zinamfanya aruhusiwe kufanya hivyo, kama vile kutopata maji kabisa, au uchache wake pamoja na kuwepo na hitaji la kuyanywa na mfano wake.

Au kwa sababu ya kuwepo ugumu mkubwa katika kutawadha kwa maji hayo; kwa sababu ya ukali wa baridi au ugonjwa. Na haya hutokea sana katika safari. Na baridi inayokusudiwa hapa ni ile ambayo inampa mtu ugumu kwa namna kwamba kuna dhana kubwa kwamba atapata ugonjwa au kuchoka sana kwa sababu ya kuyatumia. Baridi ya kawaida hiyo siyo sababu ya kufanya tayammam.

Hilo la kutayammam linaruhusika mradi hakuna maji karibu ambayo yanaweza kuletwa, ikiwa hayapo, au kuyapasha moto ikiwa ni baridi.

Kufuta juu ya Khuff

Kupangusa juu ya Khuff ni wakati mtu amevalia viatu vya ngozi nyepesi ambavyo vinafunika miguu, au amevalia soksi au mfano wake miongoni mwa vitu ambavyo vinafunika miguu yote, kwa sharti kwamba alivivaa hali ya kuwa yeye mwenyewe ni safi kutokana na hadathi kubwa na ndogo. Kwa hivyo, anapopangusa kichwa chake na masikio yake anapotawadha, haimlazimu kuvua Khuff zake ili aoshe miguu yake, badala yake atapangusa tu juu ya miguu yake kwa juu ya Khuff hizo.

Ili kupangusa juu ya Khuff kuwe sahihi ni sharti kwamba zivaliwe hali ya zenyewe ni safi, zifunike miguu, na kwamba mtu azivae baada ya kutawadha kikamilifu ambapo aliosha miguu yake. Na anaweza kufuta juu yake - ikiwa aliendelea kuzivaa - kwa muda wa mchana mmoja na usiku ikiwa si msafiri, na mchana tatu na usiku wake ikiwa ni msafiri.

Ni lazima azivue Khuff ikiwa anataka kutawadha baada ya muda wa kufuta juu yake kwisha, au ikiwa analazimika kuoga - kwa sababu ya janaba na mfano wake - au ikiwa alizivaa bila kufanya usafi kamili. Basi hapo atajitahirisha kikamilifu pamoja na kuosha miguu.

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani