Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Mbinu za kujikingia za kisheria

Pamoja na kufanya visababishi vya kihisia kwa ajili ya kujizuia na kujitibu kama watu wengine, Muislamu hufanya kinga za kisheria na za kujitibu kwazo kutokana na magonjwa ya kihisia na yasiyokuwa ya kihisia. Kwa hivyo, tutajifunza baadhi yake katika somo hili.

  • Kujifunza kinga za kisheria dhidi ya magonjwa na milipuko.

Mbinu za kujikingia za kisheria

Pamoja na kuongezeka kwa wimbi la hofu kati ya watu kutokana na maradhi na magonjwa ya milipuko, Muislamu, pamoja na kuzingatia sababu za kihisia, pia anajikinga kwa kufanya visababishi vya kisheria.

1. Kumkimbilia Mwenyezi Mungu

Jambo la kwanza na muhimu zaidi ambalo muumini anajikinga kwalo katika majanga na misiba ni kumkimbilia Mwenyezi Mungu na kujikinga kwake katika kuzuia dhiki hizo. Yusuf, amani iwe juu yake, wakati mke wa Mheshimiwa yule wa Misiri alipomtamani kinyume cha nafsi yake: "(Yusuf) akasema: Audhubillahi (Najikinga na Mwenyezi Mungu)." (Yusuf: 23) Na Mariam, amani iwe juu yake, wakati Jibril alipojifananisha kwake sawa na mtu: (Maryamu) akasema: "Hakika mimi ninajikinga kwa Mwingi wa rehema aniepushe nawe." (Maryam: 18)

2. Kuomba dua kwa wingi:

Kuomba Mwenyezi Mungu dua kwa unyenyekevu, kujidhalilisha na kuonyesha kuhitaji kwake, ili aondoe balaa na wasiwasi hiyo. Kwani dua ndiyo ngome na silaha ya Mwislamu. Kwa maana balaa hiyo ilitokana na mipangilio ya Mwenyezi Mungu, basi hakuna kinachoweza kuizuia isipokuwa dua. Amesema Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Hakuna kinachoweza kuzuia mipangilio ya Mwenyezi Mungu isipokuwa dua." (Tirmidhi 2139)

3. Kushikamana na Qur-ani Tukufu

Mtu anapaswa kutafuta ponya kwayo, kwani ndiyo dawa ya magonjwa yote ya kihisia na yasiyokuwa ya kihisia. (Al-Israa: 82) Kwa imani, yakini na ukweli, sababu za uponyaji huongezeka kwa sababu ya maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Sema: Hii Qur-ani ni uwongofu na poza kwa wenye kuamini." (Fussilat: 44)

Qur-ani yote ni uponyaji. Lakini baadhi ya sura na aya zina fadhila maalumu kuliko zingine; kama vile Suratul-Fatiha, suratul-Falaq, Suratun-Nas, na Ayatul-Kursi. Ibn Al-Qayyim, Mwenyezi Mungu amrehemu, alisema: "Kama mja angejitibu vizuri na Al-Fatiha, basi angeona athari yake ya ajabu katika uponyaji. Nilikaa Makka kwa muda na nikagonjeka, na sikuweza kupata daktari wala dawa. Kwa hivyo nilikuwa nikijitibu kwa Al-Fatiha, na ninaiona ikiwa na athari ya ajabu, kwa hivyo nikawa ninamwelezea hivyo mtu ambaye anaumwa; na wengi wao walikuwa wakipona haraka."

4. Kudumu kuswali swala tano pale zinapoadhiniwa.

Hasa, swala ya Fajr, kwa kauli ya Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Mwenye kuswali (swala ya) Subhi, basi atakuwa katika ulinzi wa Mwenyezi Mungu." (Muslim 657)

5. Kuomba dua wakati unapomuona mtu mwenye balaa

Miongoni mwa ngome muhimu ni kuomba dua wakati unawaona wagonjwa na watu wenye balaa. Katika hadithi, Nabii alisema: "Yeyote anayemwona mtu anayeteseka, na akasema: 'Sifa njema ni za Mwenyezi Mungu ambaye ameniepusha na kile alichokupa mtihani, na akaniboresha mimi kuliko wengi miongoni mwa aliowaumba,' basi hatapatwa na balaa hiyo." (Tirmidhi 3432).

6. Kudumisha nyiradi za asubuhi na jioni:

Katika kudumisha kumdhukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kuna heri nyingi katika maisha haya na malipo makubwa katika Akhera. Na nyiradi za asubuhi na jioni ni miongoni mwa nyiradi muhimu zaidi ambazo Muislamu anapaswa kuzidumisha. Miongoni mwa faida zake ni: kukunjuka kwa kifua, utulivu wa moyo, kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu, na Mwenyezi Mungu kumtaja mja huyo mbele ya waja watukufu wa juu.

Miongoni mwa dua, nyiradi na kinga za kisheria ni kama ifuatavyo:

Kusoma Ayatul-Kursi kabla ya kulala:

Imekuja katika Hadithi kwamba msemaji mmoja alimwambia Abu Huraira, Mwenyezi Mungu amridhie: "Kila wakati unapoenda kwenye malazi yako (kulala), soma Ayatul-Kursi; Mwenyezi Mungu atakuekea mlinzi ambaye ataendelea kuwa pamoja nawe, na hakuna shetani yeyote atakayekukaribia mpaka ufike asubuhi." Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, akasema: "Hakika yeye amekwambia ukweli, ingawa yeye ni mwongo wa waongo. Huyo alikuwa Shetani." (Al-Bukhari 3275)

Kusoma aya mbili za mwisho za Surat Al-Baqara:

Imesimuliwa kutoka kwa Abu Mas'ud, Mwenyezi Mungu amridhie, kuwa: Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alisema: "Mwenye kusoma zile aya mbili za mwisho za Suratul Baqara usiku, basi zitakuwa ni zenye kumtosheleza." (Bukhari 5008, Muslim 808)

Kumsifu Mwenyezi Mungu kwa wingi, na kuomba msamaha:

Ikiwa mja atadumu katika kumsifu Mwenyezi Mungu na kumuomba msamaha, basi Mwenyezi Mungu atamwondolea shari na balaa. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: "Na Mwenyezi Mungu hakuwa wa kuwaadhibu nawe umo pamoja nao, wala Mwenyezi Mungu si wa kuwaadhibu na hali ya kuwa wanaomba msamaha." (Al-Anfal: 33)

Kinga zingine za kisheria:

١
Imesimuliwa kutoka kwa 'Uthman bin 'Affan, Mwenyezi Mungu amridhie, kuwa alisema: "Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, akisema: 'Mwenye kusema, 'Kwa jina la Mwenyezi Mungu ambaye hakiwezi kudhuru chochote pamoja na jina lake katika ardhi na mbinguni, naye ni Mwenye kusikia, anijuaye zaidi;" mara tatu, basi hutasibiwa na balaa kwa ghafla mpaka afike asubuhi. Na mwenye kusema hivyo anapofika asubuhi, mara tatu basi hatasibiwa na balaa kwa ghafla mpaka afike jioni. (Abu Dawud 5088)
٢
Imesimulia kutoka kwa Abu Huraira kuwa alisema: Mwanamume mmoja alimjia Nabii,rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, na akasema, "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Sikupata raha yoyote usiku wa jana kwa sababu nge aliniuma." (Mtume) Akasema, "Ama lau kuwa ulisema ulipofika jioni, 'A'udhu bikalimatillahit-tammati min sharri ma khalaq (Najilinda kwa maneno ya Mwenyezi Mungu yaliyokamilika ambayo hayapiti mwema wala muovu, na shari ya alichokiumba),' basi hangekudhuru." (Muslim 2709).
٣
Imesimuliwa kutoka kwa 'Abdallah bin Khubaib, Mwenyezi Mungu amridhie, kuwa alisema: "Tulitoka katika usiku mmoja wenye mvua na giza tukamtafuta Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, ili atuswalishe. Kisha Nikamfikia, naye akasema: 'Sema.' Lakini sikusema chochote. Kisha akasema: 'Sema.' Lakini sikusema kitu. Akasema: 'Sema.' Kwa hivyo nikasema: Niseme nini?" Akasema, "Sema: Mwenyezi Mungu ni wa pekee, na suratul-Falaq na suratun-Nas wakati unaamka mara tatu, hizo zitakutosheleza na kila kitu." (Tirmidhi 3575)
٤
Imesimuliwa kutoka kwa 'Abdullah bin Umar, Mwenyezi Mungu amridhie, kwamba alisema: Katika dua za Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, ilikuwa ni, "Allaahumma innii a’udhu bika min-zawaali ni’matika, watahawwuli ‘aafiyatika, wafujaa-ati niqmatika, wajamii’i sakhatwika (Ewe Mwenyezi Mungu! Hakika mimi ninajikinga kwako kutokana na kuondokewa na neema zako, na kubadilika kwa afya yako, na adhabu yako ya ghafla, na hasira zako zote)." (Muslim 2739)
٥
Imesimuliwa kutoka kwa Anas, Mwenyezi Mungu amridhie, kwamba Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alikuwa akisema: "Ewe Mwenyezi Mungu, najikinga kwako kutokana na ukoma, wazimu, na shari ya magonjwa mabaya." (Abu Dawud 1554)

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani