Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Kumuosha maiti na kumvalisha sanda

Sheria ya Kiislamu inamheshimu Mwislamu baada ya kifo chake kama inavyomheshimu wakati wa uhai wake. Katika somo hili, utajifunza baadhi ya hukumu zinazohusiana na kuosha na kumvalisha maiti sanda.

  • Kujua nini kinapendekezwa kufanywa baada ya kifo cha Mwislamu.
  • Kujua utaratibu wa kumuosha maiti.
  • Kujua baadhi ya masharti ya kumvisha maiti sanda.

Ni nini kinapendekezwa kufanya Muislamu anapokufa?

Kifo cha mtu kinapothibitishwa, na roho ikawa imetengana na mwili, inapendekezwa kufanya mambo kadhaa.

1. Kufumba macho ya marehemu kwa upole na heshima

Mtume, rehema na amani za Mweneyzi Mungu zimshukie, alipoingia alimokuwa Abu Salama huku macho yake yako wazi, alimfumba macho na akasema: “Mnapowahudhuria maiti wenu, basi wafumbeni macho.” (Ibn Majah 1455)

2. Uvumilivu na kujidhibiti nafsi

Mtu haruhusiwi kuinua juu sauti wakati wa kulia na kuomboleza. Bali anafaa kuwatia subira jamaa na familia ya maiti. Mtume, rehema na amani zimshukie, alimuamuru mmoja wa mabinti zake ambaye mtoto wake mchanga alikuwa amekufa kwamba awe na subira na atarajie malipo kutoka kwa Mwenyezi Mungu. (Al-Bukhari 1284, Muslim 923)

3. Kumuombea rehema na msamaha, na kuwaombea familia yake subira na faraja

Kama Mtume, rehema na amani zimshukie alivyomfanyia Abu Salama, mmoja wa maswahaba wake watukufu alipofariki, na akasema: “Hakika, roho inapochukuliwa, macho yanaifuata." Kisha akasema, "Ewe Mwenyezi Mungu! Msamehe Abu Salama, na ipandishe daraja yake katika waongofu, na uweke badili yake kwa aliyowacha nyuma, na utusamehe sisi na yeye, ewe Mola Mlezi wa walimwengu wote, na umkunjulie katika kaburi lake, na umtilie mwangaza ndani yake.” (Muslim 920)

4. Kuharakisha maandalizi ya marehemu, kumuosha, kumswalia na kumzika

Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za mwenyezi Mungu zimshukie: “Iharakisheni jeneza. Ikiwa ni mtu mwema, basi ni heri mnayoitanguliza kwake. Na ikiwa ni kinyume chake, basi hiyo ni shari (mliyoibeba, na ambayo mnatakiwa kwa haraka) muishushe kutoka kwenye shingo zenu." (Al-Bukhari 1315, Muslim 944)

5. Kuwasaidia wana familia ya maiti

Inafaa wasaidiwe kwa kuwatekelezea baadhi ya majukumu yao. Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, aliamrisha waandaliwe chakula familia ya binamu yake Jafar bin Abi Talib alipouawa, Mwenyezi Mungu amuwie radhi. Mtume alisema: “Watengenezeeni chakula familia ya Jaafar, kwani limewafikia jambo la kuwashughulisha.” (Abu Dawud 3132, Tirmidhi 998, na akasema kwamba ni sahihi, na Ibn Majah 1610)

Kumuosha maiti

Ni lazima maiti aoshwe kabla ya kuvikwa sanda na kuzikwa. Ataoshwa na mmoja wa familia yake, jamaa yake, au Waislamu wengineo. Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, alioshwa alipofariki, ilhali yeye ndiye safi zaidi aliyesafishwa na Mwenyezi Mungu.

Namna ya kumuosha maiti:

Katika kuosha maiti, inafaa kueneza maji kwenye mwili mzima, kumuondolea uchafu wowote ikiwa utapatikana, pamoja na kujali sana suala la kusitiri sehemu zake za siri wakati wa kumuosha. Inapendekezwa kuzingatia mambo yafuatayo:

1. Kufunika sehemu zake za siri: kati ya kitovu chake na magoti yake, baada ya kumvua nguo zake.

2. Muoshaji atavaa glavu au kitambaa kwenye mkono wake wakati wa kuosha sehemu za siri za maiti.

3. Kuanza kwa kuondoa uchafu na najisi kutoka kwenye mwili wa maiti.

4. Kisha huosha viungo vya wudhuu kwa utaratibu wake sahihi unaojulikana.

5. Kisha kuosha kichwa chake na mwili wote. Inapendekezwa kuuosha kwa mkunazi au kwa sabuni, na kisha atamiminiwa maji baada ya hayo.

6. Inapendekezwa kuosha kwanza upande wa kulia, kisha upande wa kushoto.

7. Inapendekezwa kumuosha mara tatu au zaidi ikiwa kuna haja ya kufanya hivyo.

Kama alivyowaambia Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, wale wanawake waliokuwa wanamuosha binti yake, Zainabu, Mwenyezi Mungu amridhie: "Mwosheni mara tatu au tano au zaidi mkiona ni sawa kufanya hivyo." (Al-Bukhari 1253, Muslim 939)

8. Kumuwekea kitambaa au pamba

Inawezekana kumuwekea kitambaa au pamba katika tupu ya nyuma, ya mbele, masikio, pua na mdomo; ili uchafu au damu inayotoka ndani yake isitoke.

9. Kumpaka maiti manukato

Inapendekezwa kumpaka maiti manukato wakati wa kumwosha na baada ya kumwosha. Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, aliwaamrisha wale waliokuwa wanamuosha binti yake, Zainab kwamba watie kafuri katika muosho wa mwisho. (Al-Bukhari 1253, Muslim 939)

Ni nani anayefaa kumwosha maiti?

١
Ikiwa maiti atausia kwamba aoshwe na fulani, basi wasia wake utatekelezwa.
٢
Wanaume na wanawake walio chini ya umri wa miaka saba, inajuzu kuoshwa na wanaume au wanawake, ingawa ni bora kwa kijana kuoshwa na wanaume na msichana kuoshwa na wanawake.
٣
Ikiwa maiti ana zaidi ya miaka saba, basi mwanamume ataoshwa na wanaume tu na mwanamke ataoshwa na wanawake.
٤
Inaruhusika kwa mume kumuosha mke wake na mke kumuosha mumewe. Ali bin Abi Talib alimwosha Fatima, Mwenyezi Mungu awe radhi nao wote wawili.

Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake alisema: “Lau ningeweza kujua hali yangu ya mbeleni, yale ambayo nimeshajua, basi Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, asingeoshwa na yeyote isipokuwa wake zake.” (Abu Dawud 3141 Ibn Majah 1464)

Kuvikwa maiti sanda

Kumkafini maiti kwa vazi linalomsitiri ni katika ya haki za wajibu kwake juu ya familia yake na waislamu wote. Nayo ni faradhi ya kutoshelezana, kwa kauli ya Mtume, rehema na amani zimshukie: "Vaeni katika nguo zenu ambazo ni nyeupe. Kwani hizo ndizo bora katika nguo zenu, na wakafinini kwazo maiti wenu." (Abu Dawud 3878)

Gharama za sanda zinachukuliwa kutoka katika mali yake ikiwa ana mali. Na ikiwa hataacha mali, basi gharama za sanda yake ni wajibu kwa wale ambao ni wajibu wao kumsaidia hali ya hai wake, kama vile baba yake, babu, mwanawe na mwana wa mwanawe. Lakini ikiwa hawana uwezo wa kufanya hivyo, basi hilo litawalazimu Waislamu matajiri.

Inatosha kuwa sanda chochote kinachositiri mwili wa maiti kiwe miongoni mwa nguo safi, sawia awe maiti ni mwanamume au mwanamke.

Inapendekezwa wakati wa kukafini maiti:

١
Mwanamume kuvikwa sanda tatu nyeupe. Kama Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu, alivyovikwa sanda. Na inapendekezwa kwa mwanamke kuvikwa sanda tano nyeupe ili kumsitiri zaidi.
٢
Inapendekezwa kwamba rangi ya sanda iwe nyeupe ikiwa ni rahisi kupata, kwani Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie alisema: "Vaeni katika nguo zenu zile ambazo ni nyeupe. Kwani ni katika nguo zenu bora, na wakafinini kwazo maiti wenu." (Abu Dawood 4061, Tirmidhi 994 na akasema kwamba ni sahihi, Ibn Majah 3566)
٣
Inapendekezwa kuipaka sanda manukato kwa aina zinazoruhusiwa za manukato.
٤
Inafaa kufanya bidii katika kumvisha maiti sanda upande wa kichwa na miguuni. Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, alisema: “Mmoja wenu anapomkafini ndugu yake, basi na amkafini vizuri.” (Muslim 943).

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani