Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Maisha ya Nabii Muhammad, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake

Kujua maisha ya Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, ni katika dini. Katika somo hili, utajifunza mengi katika maisha yake, kabla ya Mwenyezi Mungu kumpa utume.

  • Kujua mambo muhimu zaidi ya maisha ya Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, tangu kuzaliwa kwake hadi muda mfupi kabla ya utume.

Maisha ya Nabii

Inamlazimu Muislamu kujua kwa kina maisha ya Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, ili aweze kumuiga katika mambo yote ya maisha yake, kwani maisha yake yalikuwa ni utekelezaji wa hukumu za Uislamu na sheria zake. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Hakika nyinyi mnayo ruwaza njema kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa anayemtaraji Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho." (Al-Ahzab: 21)

1. Nasaba ya Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake

Nasaba ya Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, ndiyo nasaba bora zaidi na tukufu zaidi. Yeye ni Muhammad ibn 'Abdillah, ibn 'Abdul-Muttalib ibn Hashim, ibn 'Abd Manaf, ibn Qusay, ibn Kilab, ibn Murra, ibn Ka'b, ibn Lu'ay, ibn Ghalib, ibn Fihr, ibn Malik, ibn an-Nadhr, ibn Kinana, ibn Khuzayma, ibn Mudarika, ibn Ilyas, ibn Mudhar, ibn Nizar, ibn Ma'd ibn Adnan. Naye Adnan ni katika wana wa Ismail, amani iwe juu yake.

2. Wazazi wake

Baba yake ni Abdullah bin Abdul Muttalib bin Hashim. Alifariki hali ya kuwa Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, bado yuko tumboni mwa mama yake.

3. Kuzaliwa kwake

Alizaliwa Jumatatu katika mwezi wa Rabi 'al-Awwal, mwaka wa tembo, unaolingana na 571 miladiya.

4. Kunyonyeshwa kwake

Alinyonyeshwa siku kadhaa na Thuwaiba, kijakazi wa Abu Lahab, kisha akanyonyeshwa na Halima as-Saadiya kutoka kwa Bani Sa'd, na akaishi naye huko katika Bani Sa'd kwa miaka minne takriban. Moyo wake ulipasuliwa huko, na fungu la shetani likatolewa katika nafsi yake, kisha Halima akamrudisha kwa mama yake baada tu ya hilo kufanyika.

5. Malezi na ujana wake

١
Baada ya Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kurudi kutoka katika makazi ya Bani Sa'd kwenda kwa mama yake huko Makka, akainukia chini ya malezi yake. Kisha mama yake akafia huko Al-Abwa, hali ya kuwa anarudi kutoka Madina kwenda Makka, ilhali umri wa Nabii hapo ni miaka sita. Hivyo ndivyo alivyoishia kuwa yatima bila ya baba wala mama.
٢
Babu yake, Abdul Muttalib alimrudisha Makka, akamtunza na kumlea, na alipomaliza miaka minane, miezi miwili na siku kumi babu yake, Abdul Muttalib akafia huko Makka.
٣
Baada ya kifo cha babu yake, ami yake, Abu Talib akamtunza na kumlea pamoja na wanawe, na hata akampendelea zaidi yao, akampa heshima maalumu, na akaendelea kumlinda kwa zaidi ya miaka arobaini.

Kazi yake kabla ya kupewa utume

١
Katika udogo wake alikuwa akichunga kondoo huko Makka kwa malipo ya Qiraat.
٢
Alipofika umri wa miaka kumi na miwili, alitoka pamoja na ami yake Abu Talib kwenda katika safari ya kibiashara huko Sham. Na alipofika umri wa miaka ishirini na tano, Khadija binti Khuwaylid - ambaye alikuwa mfanyabiashara wa Kiquraishi mwenye heshima na mali - alimpa ruhusa ya kutoka na mali yake kwenda huko Sham ili aifanyie biashara. Hilo ni kwa sababu ya yale aliyosikia kuhusu ukweli wa Nabii katika mazungumzo yake, amana yake kubwa na tabia yake tukufu. Kwa hivyo, Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, akakubali hilo na akatoka na mali yake pamoja na mtumishi wa Khadija aitwaye Maysara. Aliporudi Makka, Khadija akaona amana kubwa na baraka katika mali yake kiwango ambacho hakuwahi kuona hapo awali.

Maisha yake kabla ya kupewa utume

Maisha ya Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, kabla ya utume yalikuwa maisha mema na matukufu ambayo hayakuwa na mapungufu yoyote wala makosa. Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, aliinukia hali ya kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu amemzunguka na ulezi wake akimlinda kutokana na uchafu wa zama za ujinga, mpaka akawa mbora zaidi wa watu wake katika mwenendo, tabia na mtukufu zaidi wa hadhi, ujirani, ustahamilivu, mkweli wao zaidi katika mazungumzo, mwenye amana kubwa zaidi, wa mbali wao zaidi na machafu na tabia zenye kuchafua wanaume, mpaka akajulikana kwao kwamba yeye ni “mkweli na mwaminifu."

6. Wake wa Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake

Mtume, rehema na amani zimshukie, alimwoa Khadija, Mwenyezi Mungu amuwie radhi, alipofikia umri wa miaka ishirini na tano, alipotoka kwenda huko Sham kufanya biashara pamoja na mtumishi wake Khadija aitwaye Maysara. Basi Maysara akaona cha kumshangaza mno kuhusiana na mambo yake, kama vile ukweli na uaminifu. Aliporudi, akamjulisha bibi yake yale aliyoyaona. Basi Khadija akataka amuoe. Na yeye ndiye aliyekuwa mwanamke wa kwanza ambaye Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake alioa, na hakuwahi kumuoa mwengine mpaka Khadija alipokufa. Naye Khadija, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake alikuwa ndiye mama wa watoto wake wote isipokuwa Ibrahim. Na alifariki miaka mitatu kabla ya Hijra.

Majina ya wake za Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake

١
Khadija, Mwenyezi Mungu awe radhi naye.
٢
Alipokufa Khadija Mwenyezi Mungu amridhie, Nabii alimuoa Sauda binti Zam'a, Mwenyezi Mungu amridhie.
٣
Kisha akamuoa Aisha bint Abu Bakr As-Siddiq, Mwenyezi Mungu awe radhi nao.
٤
Kisha akamuoa Hafsa bint Umar bin Khattab, Mwenyezi Mungu awe radhi nao.
٥
Kisha akamuoa Zainab bint Khuzayma bin Al-Harith, Mwenyezi Mungu amridhie.
٦
Na pia alimuoa Umm Salama, ambaye jina lake ni Hind bint Umayya, Mwenyezi Mungu awe radhi naye.
٧
Pia alimuoa Zainab binti wa Jahsh, Mwenyezi Mungu awe radhi naye.
٨
Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu akamuoa Juwayriya bint Al-Harith, Mwenyezi Mungu amridhie.
٩
Kisha akamuoa Umm Habiba, Mwenyezi Mungu amridhie, na jina lake lilikuwa Ramla, na ilisemekana kuwa jina lake ni Hind bint Abu Sufyan.
١٠
Na alioa baada ya ushindi wa Khaybar Safiya bint Huyay bin Akhtab, Mwenyezi Mungu amridhie.
١١
Kisha akamuoa Maimuna bint Al-Harith, Mwenyezi Mungu amridhie. Na yeye ndiye wa mwisho miongoni mwa wake za Mtume wa Mwenyezi Mungu.

7. Watoto wa Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake

Watoto wake ni saba kulingana na kauli iliyo sahihi: watatu wa kiume na wanne wa kike.

Watoto wake wa kiume ni watatu: Al-Qasim, na Nabii aliitwa jina lake la utani kwa huyu mwanawe, lakini aliishi siku chache tu kisha akafa. Na Abdullah ambaye alipewa jina la utani la At-Twahir (aliye safi), At-Tayyib (mzuri). Na katika watoto wake pia ni Ibrahim.

Binti zake ni wanne: Zainab, ambaye ndiye binti yake mkubwa, Ruqayya, Umm Kulthum na Fatima. Kwa hivyo, watoto wa kiume na wa kike wa Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, wote walikuwa kutoka kwa mkewe, mama wa waumini, Khadija, Mwenyezi Mungu amridhie, isipokuwa Ibrahim. Kwani yeye alikuwa kutoka kwa suria wa Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, anayeitwa Mariya, mwanamke wa Kikoptiki, ambaye Muqawqas alimpa Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani