Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Maadili ya Kiislamu katika Miamala inayohusiana na mali

Katika somo hili, tutajifunza kuhusu baadhi ya maadili yanayohitajika katika miamala ya inayohusiana na mali.

  • Kujifunza kuhusu maana ya miamala inayohusiana na mali katika Uislamu.
  • Kuonyesha ubora wa Sheria ya Kiislamu katika mlango wa miamala inayohusiana na mali.
  • Kubainisha maadili ya Kiislamu ambayo ni lazima yazingatiwe katika miamala inayohusiana na mali.

Maadili yanahusiana kwa ukaribu na mambo yote ya maisha. Miongoni mwa mambo muhimu zaidi yanayoutofautisha mfumo wa kifedha wa Kiislamu na mifumo mingineyo ni maadili yaliyo ndani yake na ambayo inayatunza. Hili ndilo linaloufanya mfumo wa kifedha wa Kiislamu kuwa wa kipekee kuliko mifumo mingineyo.

Miamala inayohusiana na mali katika Uislamu

Ni ambayo yote ambayo Sheria ya Kiislamu inaruhusu kufanya ili kuchuma mapato halali. Yanajumuisha shughuli zinazohusiana na mali zinazojumuisha mikataba yote ambayo inategemea mali au haki za kimali zinatokana nazo. Kama vile uuzaji, ununuzi, kukodisha, kampuni, na mikataba mingineyo. Hukumu zinazohusiana na miamala ya Kiislamu ni hukumu za kisheria zinazodhibiti miamala ya watu ya kimali na kiuchumi.

Malengo ya miamala ya kimali ya Kiislamu

١
Inahakikisha kufikia kumridhisha Mwenyezi Mungu; kwa kutii amri yake ya kutembea katika ardhi. Amesema Aliyetakasika: "Yeye ndiye aliyeidhalilisha ardhi kwa faida yenu. Basi tembeeni katika pande zake, na kuleni katika riziki zake. Na kwake Yeye ndiyo kufufuliwa." [Al-Mulk: 15]
٢
Kuchuma mali na kupata riziki ambayo inahakikisha kuendelea kwa maisha, na kuongeza mali ili kufikia manufaa, masilahi na raha zinazoruhusiwa za kiulimwengu.
٣
Kufikia hadhi ya juu Peponi, kwa kujitahidi kutafuta vya halali na kujiepusha vya haramu katika miamala yote. Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema: "Mfanyabiashara mkweli, mwaminifu atakuwa pamoja na Manabii, Wakweli na wale waliouawa kwa ajili ya Dini." (Tirmidhi 1209)
٤
Kutumia mali kulingana na maelekezo ya kisheria ambayo yanadhamini kujenga jamii njema, yenye uwezo wa kukua na kuendelea.
٥
Kukidhi mahitaji ya wanajamii wote, ambayo huwasaidia kufikia aliyoyataka Mwenyezi Mungu kutoka kwao, na kumuabudu Mwenyezi Mungu aliyetakasika katika matendo yao na maneno yao.
٦
Kushika usukani vyema katika ardhi, na kuiimarisha kwa mujibu wa sheria ya Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu alisema: "Naye ndiye aliyekufanyeni makhalifa wa duniani, na amewanyanyua baadhi yenu juu ya wengine daraja kubwa kubwa, ili akujaribuni kwa hayo aliyokupeni. Hakika Mola Mlezi wako ni Mwepesi wa kuadhibu, na hakika Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu." [Al-An'am: 165].

Hali ya wastani ya miamala ya Kiislamu

Uislamu ndiyo dini ya haki. Dini hii ilileta mambo yaliyo sawa kwa watu na yenye kuwaboresha; kwa sababu ilitoka kwa Muumba wa watu, Mtukufu, aliye juu, anayewajua zaidi na anayajua yenye kuwanufaisha. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: "Je, aliyeumba hajui, naye ndiye Mjua siri, Mwenye habari?" [Al-Mulk: 14] Tofauti na sheria na mifumo mingine, Uislamu umekuja na mfumo unaohusiana na mali ambao unazingatia mahitaji ya mwili na mambo ya kidunia, na pia unazingatia mahitaji ya kiroho na mambo ya akhera.

Kwanza: Upande wa kidunia: Sheria ya Kiislamu ilidhibiti miamala ya watu inayohusiana na mali kwa njia ambayo inafanikisha uadilifu kati ya hao wanaoamiliana, na kwa njia ambayo inampa kila mwenye haki haki yake, na kuwapa wote utoshelevu. Vile vile ilipanua mlango wa halali katika miamala, na ikaharamisha kila kitu ambacho kinamdhuru mmoja wa hao wanaoamiliana.

Pili- Upande wa kidini: Lengo kuu la hukumu zote za kisheria ni kufikia ridha ya Mwenyezi Mungu na kupata Pepo. Kwa kuongezea, hukumu za miamala ya Kiislamu kunaleta udugu miongoni mwa waumini kwa kueneza uadilifu na kuhimiza hisani, kama vile kumpa muhula mwenye ugumu wa kulipa deni, na kuharamisha kila yenye kuleta chuki katika vifua, kama vile riba na kamari.

Mifano ya miamala inayohusiana na mali kwa kuzingatia haki mbalimbali

Kwanza - Uadilifu: Hili ndilo huhakikisha kwamba kila mmoja wa pande mbili ziinazoamiliana zinapata haki yake bila kuongezewa wala kupunguziwa, kama vile kuuza au kukodisha kwa bei inayofaa. Mwenyezi Mungu alisema: "Lakini Mwenyezi Mungu ameihalalisha biashara." (Al-Baqarah: 275). Pili - Fadhila: Nayo ni hisani; kama vile kumpa muhula mwenye ugumu katika kulipa deni au hata kumuondolea deni lote. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: "Na akiwa (mdaiwa) ana shida, basi (mdai) angoje mpaka afarijike. Na mkiifanya deni kuwa ni sadaka, basi ni bora kwenu, ikiwa mnajua." [Al-Baqarah: 280] Na kama vile kukubaliana na mfanyakazi juu ya mshahara na kisha ukampa zaidi yake. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: "Na fanyeni wema. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao wema." [Al-Baqarah: 195]

Tatu - Dhuluma: Ni mtu kupata zaidi ya haki yake, na kula mali za watu kwa batili; kama vile riba, kamari, kumnyima mfanyakazi haki yake na mengineyo. Mwenyezi Mungu alisema: "Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na acheni riba zilizobakia, ikiwa nyinyi ni Waumini. Basi msipofanya, jitangazieni vita na Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Na mkitubu, basi haki yenu ni rasilmali zenu. Msidhulumu wala msidhulumiwe." (Al-Baqara: 278-279) Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alisema: "Mwenyezi Mungu amesema: "Nitakuwa hasimu dhidi ya watu watatu Siku ya Kiyama: 1. Mtu anayefanya agano kwa Jina langu, kisha akalivunja (akasaliti). 2. Mtu aliyemuuza mtu huru (kama mtumwa) na akala thamani yake 3. Mtu aliyeajiri mfanyakazi, na akamfanyia kazi kikamilifu, lakini yeye hakumlipa mshahara wake." (Al-Bukhari 2227)

Miongoni mwa maadili ya miamala ya Kiislamu inayohusiana na mali (1):

١
Kushikamana na kutimiza mikataba inayoruhusiwa. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: "Enyi mlioamini, timizeni mikataba." [Al-Maidah: 1]
٢
Kutekeleza amana. Mwenyezi Mungu alisema: "Basi aliyeaminiwa airudishe amana ya mwenzake, na amche Mwenyezi Mungu, Mola wake Mlezi." [Al-Baqarah: 283]
٣
Kutoficha ushahidi. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Wala msifiche ushahidi. Na atakayeuficha, basi hakika moyo wake ni wenye kutenda dhambi. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi zaidi wa mnayoyatenda." [Al-Baqarah: 283]
٤
Ukweli na ushauri: Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alisema juu ya wawili wanaofanya baishara: "Ikiwa watasema ukweli na wakabainisha kasoro na sifa nzuri (za bidhaa zao), basi watabarikiwa katika mauziano (mabadilishano) yao. Na ikiwa wataficha kitu au wakasema uongo, basi baraka zitaondolewa katika mauziano yao hayo." (Al-Bukhari 2079, and Muslim 1532)
٥
Kubainisha na kutodanganya na kuhadaa. Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alisema, "Na mwenye kutuhadaa si miongoni mwetu.” (Muslim 101)

Miongoni mwa maadili ya miamala ya Kiislamu ni (2):

١
Kuepuka mambo yenye utata: Haya ni mambo ambayo mtu amachanganyikiwa kujua ni ipi halali na ni ipi haramu. Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Hakika halali iko wazi na haramu iko wazi, na kati ya viwili hivyo kuna vitu vyenye shaka ambavyo wengi wa watu hawavijui. Kwa hivyo, mwenye kuepuka hivyo vyenye shaka, basi hakika atakuwa ameshaiokoa dini yake na heshima yake. Lakini Mwenye kuingia katika mambo hayo yenye shaka, ataingia katika haramu." (Al-Bukhari 52, Muslim 1599)
٢
Kutokula mali za watu kwa batili: Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Wala msiliane mali zenu kwa batili na kuzipeleka kwa mahakimu ili mpate kula sehemu ya mali za watu kwa batili, na hali mnajua." [Al-Baqarah: 188]
٣
Mwislamu anapaswa kumpendea ndugu yake kile anachojipendea mwenyewe. Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alisema: "Hataamini mmoja wenu mpaka ampendee ndugu yake (Mwislamu) kile anachoipendea nafsi yake." (Al-Bukhari 13, Muslim 45)

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani