Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Kuamini Uungu wa Mwenyezi Mungu

Mwenyezi Mungu, Mtakatifu, Mtukufu ndiye Mungu wa kweli, na kila asiyekuwa Yeye miongoni mwa miungu ni batili. Katika somo hili, utajifunza kuhusu maana ya Tauhid Al-Uluhiyya (Tauhidi ya Uungu) na umuhimu wake.

  • Kujua maana ya Tauhid Al-Uluhiyya (Tauhidi ya Uungu).
  • Kujua umuhimu wa Tauhid Al-Uluhiyya (Tauhidi ya Uungu).

Maana ya Tauhid Al-Uluhiyya (Tauhidi ya Uungu)

Ni kusadiki kithabiti kwamba Mwenyezi Mungu, Mtukufu peke yake ndiye anayestahiki kila aina ya ibada za dhahiri na za ndani. Kwa hivyo, tunampwekesha Mwenyezi Mungu katika kila aina za ibada, kama vile dua, hofu, kutegemea, kuomba msaada, Swala, Zaka na Saumu. Kwa hivyo, hakuna muabudiwa wa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Mtukufu. Kama alivyosema Mwenyezi Mungu aliyetukuka, "Mungu wenu ni Mungu Mmoja. Kwa hivyo, mwenye kutaraji kukutana na Mola wake Mlezi, basi na atende vitendo vyema, wala asimshirikishe yeyote katika ibada ya Mola wake Mlezi." (Al-Kahf: 110)

Hapa, Yeye Mtukufu akajulisha kuwa Mungu ni Mungu mmoja; yaani, muabudiwa mmoja. Kwa hivyo, hairuhusiki kuchukuliwa mungu mwingine asiyekuwa Yeye, na asiabudiwe asiyekuwa Yeye.

"Hakika mungu wenu ni Allah (Mwenyezi Mungu) tu. Hapana mungu isipokuwa Yeye. Amekienea kila kitu kwa elimu yake." (Twaha: 98)

Umuhimu wa Tauhid Al-Uluhiyya (kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika uungu wake):

Unadhihirika umuhimu wa Tauhid Al-Uluhiyya (kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika uungu wake) katika pande nyingi:

1. Kwamba ndiyo makusudio ya kuumbwa majini na wanadamu

Hawakuumbwa isipokuwa wamuabudu Mwenyezi Mungu peke yake, ambaye hana mshirika. Kama alivyosema Mtakatifu, "Nami sikuwaumba majini na watu isipokuwa kwamba waniabudu Mimi." (Adh-Dhariyat: 56)

2. Kwamba hilo ndilo kusudio katika kutumwa Mitume na kuteremshwa Vitabu.

Makusudio ya hilo ni kuwalingania viumbe wamwabudu Mwenyezi Mungu peke yake, na wakufuru vinavyoabudiwa badala yake. Kama alivyosema Mtakatifu, "Na kwa hakika, kwa kila umma tuliutumia Mtume kwamba: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na muepukeni Twaghut." (An-Nahl: 36)

3. Kwamba ndio wajibu wa kwanza juu ya mwanadamu

Kama ilivyokuja katika wasia wa Nabii - rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - kwa Mu’adh bin Jabal, Mwenyezi Mungu amuwie radhi, alipomtuma Yemen, akamwambia, “Hakika wewe, utawajia kaumu ya Watu wa Kitabu, basi na liwe jambo la kwanza utakalowalingania ni kumwabudu Mwenyezi Mungu, Mwenye Nguvu, Mtukufu.” (Bukhari 1458, Muslim 19)

4. Kwamba Tauhid Al-Ulihiyya (ya uungu) ndiyo maana halisi ya “Hakuna mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu.”

Kwa hivyo, Mungu ndiye muabudiwa. Na maana ya “hakuna mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu,” ni hakuna muabudiwa wa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo, tunamuabudu Yeye pekee, wala hatumfanyii asiyekuwa Yeye chochote katika aina za ibada.

5. Kwamba kuamini Uungu ndiyo matokeo ya kimantiki ya kuamini kwamba Mwenyezi Mungu pekee yake ndiye Muumba, Mmiliki, Mwendeshaji mambo.

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani