Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Je, mtu anaingiaje katika Uislamu?

Wakati mtu anapoingia katika Uislamu ni wakati mkubwa zaidi wa maisha yake, na ni kuzaliwa kwake kweli baada ya kujua sababu ya kuwepo kwake katika maisha haya. Somo hili linahusu kile ambacho mtu binafsi anahitaji ili kuwa Muislamu na kuingia katika dini hii kubwa.

  • Kujua jinsi ya kuingia katika Uislamu.
  • Kujua umuhimu wa toba na mambo ya kumfanya mtu kudumu ndani yake.

Mtu anaingia katika Uislamu anapotamka shahada mbili pamoja na kujua maana yake huku akiwa na yakini nazo, na kutii mambo yote yanayohitajiwa nazo.

Na shahada mbili ni:

١
Ninashuhudia ya kwamba hapana mungu ila Mwenyezi Mungu, (yaani, ninashuhudia na kuitakidi kuwa hakuna mungu anayeabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu, kwa hivyo ninamuabudu Yeye peke yake bila mshirika yeyote).
٢
Na ninashuhudia ya kwamba Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, (yaani, nashuhudia kuwa Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu aliyetumwa kwa watu wote, huku nikiyatii maamrisho yake, nikijiepusha na makatazo yake, na ninamuabudu Mwenyezi Mungu kwa mujibu wa sheria na Sunnah zake).

Kuoga kwa Mwislamu mpya:

Wakati mtu anapoingia katika Uislamu ni wakati mkubwa zaidi wa maisha yake, na ni kuzaliwa kwake kwa kweli. Baada ya hapo, anajua sababu ya kuwepo kwake katika maisha haya. Na ni jambo linaloruhusiwa kisheria anapoingia katika dini kwamba aoge na afikishe maji vyema kwenye mwili wake wote. Kama vile alivyotakasa mambo ya ndani yake kutokana na ushirikina na dhambi, inapendekezwa kwake kuitakasa sehemu yake ya nje kwa kuoga kwa maji.

Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alimuamuru Swahaba mmoja - ambaye alikuwa ni miongoni mwa viongozi wa Waarabu, – alipotaka kusilimu kwamba aoge. (Al-Bayhaqi 837)

Toba

Toba ni kurudi kwa Mwenyezi Mungu. Kila anayeacha uasi na ukafiri wake na kumrudia Mwenyezi Mungu huku akiwa mkweli moyoni mwake, basi atakuwa ametubu kwa Mwenyezi Mungu.

Masharti ya toba kuwa sahihi:

١
Kuacha dhambi: Haifai kutubia dhambi huku ukiendelea kuifanya huku ukitubia. Hata hivyo, ikiwa dhambi itarejea baada ya toba sahihi, basi toba yake iliyotangulia haibatiliki, bali anahitaji toba mpya, na kadhalika.
٢
Kujuta kwa madhambi na maasi yaliyopita: Amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Majuto ni toba." (Ibn Majah 4252) Na toba haiwezi kufikirika isipokuwa kwa mwenye kujuta na kuhuzunika. Kujuta kwa madhambi aliyoyafanya, aliyetenda na mwenye kuzungumzia madhambi yake yaliyopita na akajifakhirisha kwayo, hahesabiwi kuwa ni mwenye kujuta.
٣
Kuazimia kutorejea: Toba ya mja haiwi sahihi ikiwa ana nia ya kuirudia dhambi fulani baada ya kuitubia.
٤
Kurudisha kitu alichochukua kwa dhuluma kwa mmiliki wake ikiwa dhambi hiyo inahusiana na haki za wanadamu.

Hatua za kukaa imara katika toba

١
Kujiahidi kuwa hatarejea vile alivyokuwa kiasi cha kupepesa jicho, hata kama hali au vikwazo vitakuaje. Amesema Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: “Matatu, yule ambaye hayo yatakuwa ndani yake basi atapata utamu wa Imani." Na akataja miongoni mwake: “Na achukie kurudi katika ukafiri kama anavyochukia kutupwa ndani ya Moto." (Bukhari 21, Muslim 43)
٢
Kukaa mbali na watu na maeneo ambayo yanadhoofisha imani yake na kumjaribu kutenda dhambi.
٣
Kwamba dua kwa wingi kwa Mwenyezi Mungu kwamba amuimarishe katika dini yake mpaka kufa, kwa namna yoyote ile au lugha yoyote ile. Na katika hayo ni yale yaliyokuja katika Qur-ani na Sunnah: “Mola wetu Mlezi! Usizipotoe nyoyo zetu baada ya kwisha tuongoa" (Al-Imran: 8). Na Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alikuwa akisema: “Ewe Mwenye kugeuza nyoyo, uimarishe moyo wangu katika dini yako.” (Tirmidhi 2140)

Ni nini kinachfaa baada ya toba?

Mtu akitubia na kurudi kwa Mwenyezi Mungu, basi Mwenyezi Mungu Mtukufu husamehe madhambi yote, hata yawe makubwa kiasi gani, kwani rehema yake, aliyetakasika imeenea kila kitu. Kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Sema: Enyi waja wangu waliojidhulumu nafsi zao! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu." (Az-Zumar: 53)

Basi Muislamu hutoka baada ya toba ya kweli na iliyo sahihi hali ya kuwa hana dhambi yoyote. Bali Mwenyezi Mungu Mtukufu huwalipa wakweli, wanyenyekevu, wanaojuta sawasawa kwa malipo makubwa zaidi. Yeye huwabadilishia maovu yao yakawa matendo mema, kama Mwenyezi Mungu Mtukufu alivyosema: "Isipokuwa atakayetubu, na akaamini, na akatenda vitendo vyema. Basi hao, Mwenyezi Mungu atayabadilisha maovu yao yawe mema. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe mno, Mwingi wa kurehemu." (Al-Furqan: 70)

Yeyote aliye katika hali hii, basi anapaswa zaidi kudumisha toba hiyo na kutoa kila kitu kilicho ghali na cha thamani kubwa ili asije akaanguka tena katika mitego ya Shetani inayompelekea kurudi nyuma tena.

Utamu wa imani

Yule ambaye upendo wake Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndio upendo mkubwa zaidi kwake, na akawa anawapenda wengineo kwa kiasi cha ukaribu wao kwa Mwenyezi Mungu na usahihi wa dini yao na Uislamu wao, na akawa anakuchukia kurejea katika ukafiri aliokuwamo, na ushirikina na upotofu, kama vile anavyochukia kuchomwa na Moto, basi atapata kwamba imani ina utamu na raha moyoni mwake kutokana na kuliwazwa na kutulia anakohisi kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na kufurahia sheria ya Mwenyezi Mungu na neema zake juu yake kwa kumuongoa. Kama alivyosema Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie: “Matatu, yule ambaye hayo yatakuwa ndani yake basi atapata utamu wa Imani: Yule ambaye Mwenyezi Mungu na Mtume Wake ndio vipenzi zaidi kwake kuliko kisichokuwa wawili hao, na yule anayempenda mja, na hampendi ila tu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na yule anayechukia kurudi katika ukafiri kama anavyochukia kutupwa ndani ya Moto.” (Bukhari 21, Muslim 43)

Kushikamana na dini na subira juu ya udhia ndani yake:

Mwenye kumiliki hazina ya thamani kubwa huwania sana katika kuilinda ili isichukuliwe na mikono ya waharibifu na wezi, na huilinda kutokana na kila chenye kuiathiri. Uislamu ndiyo neema kubwa zaidi ambayo Mwenyezi Mungu humpa mwanadamu. Uislamu siyo mwelekeo wa kifikira tu au hobi anayofanya mtu wakati wowote anapotaka. Bali ni dini inayotawala maisha yote ya mtu, pamoja na harakati zake na kutulia kwake. Ndiyo maana Mwenyezi Mungu Mtukufu akamwambia Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, akimuamrisha kushikamana kwa nguvu na Uislamu na Qur-ani na kwamba asiachilie mbali chochote miongoni mwa hayo; kwa sababu yeye yuko kwenye njia iliyonyooka: "Basi wewe yashike vilivyo yale yaliyofunuliwa kwako. Hakika wewe uko kwenye njia iliyonyooka." (Az-Zukhruf: 43)

Na Muislamu hatakiwi kuhuzunika akipatwa na aina fulani ya msiba baada ya kusilimu, kwani hiyo ni desturi ya Mwenyezi Mungu katika kuwajaribu waja wake. Kwa sababu watu ambao ni bora kuliko sisi walijaribiwa kwa misiba mzito, lakini wakasubiri na wakafanya juhudi. Misiba iliwajia Manabii wa Mwenyezi Mungu kutoka kwa jamaa zao hata kabla ya watu wa mbali, lakini hawakudhoofishwa na yale yaliyowasibu katika njia ya Mwenyezi Mungu, na hawakubadilika wala kugeuka. Kwa sababu majaribu ni mtihani kutoka kwa Mwenyezi Mungu ili kuonyesha ukweli wa imani ya Muislamu na nguvu ya yakini yake. Basi ni na awe kwa daraja sawa na mtihani huo, na ashikamane vilivyo na dini hii, na amuombe Mwenyezi Mungu kama Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie alivyokuwa akiomba dua sana akisema: “Ewe Mwenye kubadilisha mioyo, uimarishe moyo wangu juu ya dini yako.” (Tirmidhi 2140)

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani