Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Haki za watoto

Katika somo hili, tutajifunza kuhusu haki za watoto juu ya wazazi.

  • Kubainisha neema za Mwenyezi Mungu kwa wazazi kwa kuwapa watoto.
  • Kubainisha kujali kwa Sheria iliyosafishwa katika suala la malezi ya watoto.
  • Kujulisha kuhusu haki muhimu zaidi za watoto kwa wazazi.

Mwenyezi Mungu aliumba mioyo ya baba na mama kutamani kuwa na watoto, na kwamba wawe salama na wenye afya njema. Haya ndiyo yaliyokuwa matamanio ya baba yetu Adam na mkewe, amani iwe juu yao. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema, "Yeye ndiye aliyewaumba katika nafsi moja; na katika hiyo hiyo akamfanya mwenzi wake, ili akae naye kwa utulivu. Na anapomuingilia, hubeba mzigo mwepesi, akitembea nao. Anapokuwa mja mzito, wote wawili humwomba Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wao: Kama ukitupa mwana mwema, hakika tutakuwa katika wanaoshukuru." [Al-A'araf: 189] Kutokea kwa matamanio haya ni neema ya Mwenyezi Mungu tu inayohitaji shukrani za daima kwa sababu yake.

Uislamu umelijali suala la watoto na kila kitu kinachohusiana nao. Katika yale yanayoashiria hilo, ni mazungumzo yaliyoko katika Qur-ani Tukufu juu ya watoto na neema ya watoto, baada ya kuzungumza juu ya umiliki wa Mwenyezi Mungu juu ya mbingu na ardhi. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema, "Ufalme wa mbingu na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu; anaumba apendavyo, anamtunukia amtakaye watoto wa kike, na anamtunukia amtakaye watoto wa kiume. Au huwachanganya wanaume na wanawake, na akamfanya amtakaye tasa. Hakika Yeye ni Mjuzi, Mwenye uweza." [Shuraa: 49, 50] Mwenyezi Mungu Mtukufu amehesabu uzao kwamba ni katika pambo la maisha ya dunia. Amesema Mtukufu, "Mali na wana ni pambo la maisha ya dunia. Na mema yanayobakia ni bora mbele ya Mola wako Mlezi kwa malipo, na bora kwa matumaini." [Al-Kahf: 46]

Sheria iliwapa watoto na malezi yao umuhimu mkubwa, kwa maana wao ndio nguzo ya siku zijazo, na kwa kutengenea kwao, ndio suala la kumuabudu Mwenyezi Mungu Mtukufu linaendelea duniani, na kunafikiwa kuiimarisha dunia kwa njia inayompendeza Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema, "Enyi mlioamini! Jilindeni nafsi zenu na ahali zenu na Moto ambao kuni zake ni watu na mawe." [Tahrim: 6] Ali, Mwenyezi Mungu awe radhi naye alisema, 'Inamaanisha wafundisheni elimu na watieni tabia nzuri.' Nabii - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie - alisema, “Mwenye kuwatunza wasichana wawili mpaka wabalehe, atakuja siku ya Kiyama, mimi na yeye (tukiwa hivi);” na akaweka pamoja vidole vyake. (Muslim 2631)

Haki za watoto juu ya wazazi

١
Haki za kimali
٢
Haki zisizo za kimali

Haki za kimali

Haki hizi ni pamoja na kuwapa makazi, chakula, vinywaji, mavazi, kuwatunza kiafya, kuwapa matumizi watoto kama ilivyoagizwa na sheria. Haki hizi ni za lazima kwa baba maadamu anaweza.

Haki zisizo za kimali

Miongoni mwa haki kubwa zaidi zisizo za kimali ambazo watoto wanazo juu ya wazazi wao, ni kuwalea malezi mema yanayosimama juu ya misingi sahihi ya dini. Kwa hivyo wanafaa kufundishwa Qur-ani Tukufu, Sunna sahihi za Mtume, maisha yake na walelewe juu ya mafundisho ya Uislamu, kwa kufanya maamrisho na kuacha makatazo, na kushikamana na maadili yake mazuri. Yote hayo ni kwa sababu ya kumtukuza Mwenyezi Mungu Mtukufu, kumpenda, kumpenda Mtume wake, amani iwe juu yake, na dini yake na sheria yake.

Kuwafanyia wana huruma kuna athari kubwa katika malezi na kunafungua ufahamu wao, mradi hilo lisifikie kuwalegeza sana kwa njia ambayo inaathiri vibaya tabia zao nzuri katika maisha. Kutokuwa na rehema kwa watoto na kuwafanyia upole, na kuamiliana nao kwa ukatili mkubwa au wazazi wao kuwawia wagumu, huenda hayo yakachangia kutia giza katika nafsi zao, kuzima moto wa werevu katika akili zao, kuwafanya kutotii na kuasi, na labda wanaweza kupotea na kuharibika.

Katika haki zisizo za kimali ni kuweka mazingira ya heshima, utulivu, na upendo katika familia, ili ugomvi wa wazazi au ndugu wakubwa usitawale, ukaja kuathiri tabia za watoto na kuwafanya kuwa katika mazingira ya hofu na chuki.

Katika haki za kihisia za watoto ni wazazi kufanya bidii kuwatafutia wana wao marafiki wazuri, na kutowaruhusu kutangamana na wale walio na tabia mbaya au tabia za kulaumiwa, kwa sababu hilo linaathiri vibaya tabia zao, na wanaambukizwa tabia mbaya.

Kuwanasihi, kuwaongoza na kuwaelekeza

Wazazi wanapaswa kukagua hali za wana wao wa kiume na mabinti zao, kuangalia tabia na matendo yao, na kuingilia kati kwa ushauri, mwongozo na kuelekeza kila inavyohitajika kufanya hivyo. Lakini ni lazima kuwepo wastani katika hilo, na haifai kuendelea kuelekeza na kuongoza hata kwa kila dogo na kubwa. Kwa maana hilo linaweza kumfanya mtoto kuchoka kusikiliza au kufuata nasiha hizo. Kwa hivyo, baba na mama wanapaswa kuchagua nyakati na njia zinazofaa za ushauri na mwongozo.

Haki za watoto juu ya wazazi

١
Haki za watoto huanza kabla ya kuzaliwa; kupitia uchaguzi wa mume mwema na mke mwema.
٢
Haki ya watoto katika kupatikana na kuishi.
٣
Haki ya watoto ya nasaba
٤
Haki ya watoto kunyonyeshwa
٥
Haki ya watoto kupata jina zuri
٦
Haki ya watoto kufanyiwa Aqiqa
٧
Haki ya watoto kutendewa haki
٨
Haki ya watoto kuwaombea dua

Kuchagua mume mwema na mke mwema

Mwanamume anapaswa kuchagua yule ambaye anadhani atakuwa mama mwema, naye mwanamke pia anapaswa kuchagua yule ambaye anadhani atakuwa baba mwema.

Haki ya watoto katika kupatikana na kuishi

١
Sheria ilikataza kuwaua watoto, jambo ambalo watu wa siku za Ujinga walikuwa wakifanya kwa kuogopa umaskini au aibu.
٢
Sheria ilikataza kujizuia kabisa kuzaa.
٣
Sheria imeharamisha kuavya mimba baada ya kijusi (fetasi) kupuliziwa roho.

Haki ya watoto ya nasaba

Ni haki ya mtoto kunasibishwa na baba yake, kwa sababu haki zote za kimali na za kihisia zinazohusiana na watoto zinafungamana na haki hii. Mwanamume hana haki ya kumkana mtoto au kukataa kujinasibisha naye isipokuwa kwa ushahidi usio na shaka.

Haki ya watoto kunyonyeshwa

Zimethibiti katika elimu ya kisasa faida mbalimbali za kiafya, kisaikolojia, na kijamii katika kunyonyesha watoto. Hilo ndilo linafaa zaidi na kamili zaidi kwa hitaji la mtoto na kinga yake, na kwa ajili ya kukua kwake kuzuri kisaikolojia na kiakili, na ni katika mambo yanayoathiri katika siku zijazo werevu wake na tabia yake, na mwingiliano mzuri na ulio salama katika mambo yatakayomkumba na hisia mbalimbali.

Haki ya watoto kupata jina zuri

Siyo haki ya daraja la pili, lakini ni katika majukumu ya kimsingi ambayo Nabii - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, - aliwahimiza maswahaba wake, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao, kama alivyokuwa akiwaamrisha waepuke kuwapa watoto majina yenye maana mbaya. Bidii hii ya Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, juu ya majina mazuri ilifikia kiwango kwamba alibadilisha majina ya baadhi ya maswahaba wake baada ya kusilimu kwao, kwa sababu ya athari zilizoko katika hilo juu yao kibinafsi na kitabia.

Haki ya watoto kufanyiwa Aqiqa

Ni kile kinachochinjwa kwa ajili ya mtoto mchanga, - kwa kusudi maalumu na masharti maalumu - ili kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu. Alisema Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, “Kila mvulana anashikiliwa rahani na aqiqa yake, ambayo huchinjwa kwa ajili yake siku ya saba. Pia atanyolewa na kupewa jina.” (Abu Dawud 2838). Na akasema, “Mvulana anachinjiwa kondoo wawili wanaotoshana, naye binti anachinjiwa kondoo mmoja." (Abu Dawud 2834)

Haki ya watoto kutendewa haki

Hilo linakuwa katika kuamiliana nao kisaikolojia na kimali, wa kiume au wa kike, na hakuna kutofautisha kati yao. Imesimuliwa kutoka kwa Nu'man bin Bashir, Mwenyezi Mungu amridhie, kuwa alisema: Baba yangu alinipa baadhi ya mali yake, lakini mama yangu 'Amra binti Rawaha akasema: Sijaridhika mpaka utakapomshuhudisha Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake. Kwa hivyo baba yangu akaenda kwa Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kumshuhudisha sadaka yangu. Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, akamwambia, "Je, ulifanya hivi kwa watoto wako wote?" Akasema, "Hapana."Akasema, "Mcheni Mwenyezi Mungu, na watendeeni watoto wenu uadilifu." Basi baba yangu akarudisha sadaka hiyo. (Bukhari 2587, Muslim 1623)

Haki ya kuwaombea dua na kutowaapiza

Mtume wa Mwenyezi Mungu - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, - alisema, "Dua tatu zinaitikiwa, hakuna shaka yoyote ndani yake: dua ya aliyedhulumiwa, dua ya msafiri, na dua ya baba kwa mwanawe." (Ibn Majah 3862) Na akasema, "Msijiapize wenyewe, wala msiwaapize watoto wenu, wala msiziapize mali zenu, ili msiafikiane na saa ambayo Mwenyezi Mungu huombwa kutoa, basi akawaitikia." (Muslim 3009)

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani