Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Kuswali na kufunga saumu katika majira ya baridi

Kuna fursa kubwa za kumkaribia Mwenyezi Mungu Mtukufu katika majira ya baridi. Katika somo hili, utajifunza kuhusu baadhi ya fursa hizi, na baadhi ya hukumu zinazohusiana na kuswali katika msimu wa baridi.

  • Kujifunza hukumu za swala katika majira ya baridi.
  • Kujua fursa za kumkaribia Mwenyezi Mungu Mtukufu katika msimu huu.

Kuadhini katika majira ya baridi

Ikiwa baridi ya msimu wa baridi itaongezeka, basi na aangalie ikiwa baridi haitawazuia watu kwenda kuswali. Basi adhana itabakia kama ilivyo.

Na ikiwa baridi ni kali sana hivi kwamba ni vigumu sana kwa watu kutoka nje, basi mwadhini atasema katika adhana yake: "Sikilizeni! Swalieni majumbani mwenu;" na hapo wanaruhusiwa kuacha kwenda kuswalia msikitini.

Nafi' alisema: Wakati mmoja katika usiku wa baridi, Ibn `Umar aliadhinia katika sehemu iitwayo Dhwajnan (jina la mlima mmoja karibu na Makka), kisha akasema: "Swalieni nyumbani mwenu." Kisha akatuambia kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alikuwa wakati wa mvua nyingi au usiku wa baridi sana wakati wa safari akimwamuru mwadhini kuadhini, kisha anasema baada ya adhana, "Alaa, Swalluu fir-rihaal (Sikizeni! Swalieni nyumbani mwenu." (Al-Bukhari 632, na Muslim 697)

Kuswali kuelekea kwenye moto au kitu cha kutia joto

Watu huwasha moto wakati wa majira ya baridi, na inaweza kuwa kwamba moto huo uko kwenye Qibla ya watu hao. Na ni bora zaidi kwamba moto huo usiwe kwenye Qibla, ili kuwa mbali na kujifananisha na Majusi wanaoabudu moto, na kwa sababu unawaghafilisha wale wanaoswali. Kwa hivyo, wakiuhitaji ili kujitilia joto au ikiwa ni vigumu kubadilisha mahali hapo, basi hakuna ubaya wowote.

Ama kuswali kuelekea upande wa hita ambayo haina miale ya moto. Basi hakuna ubaya wowote kuielekea wakati wa kuswali.

Kuunganisha swala mbili

Kuunganisha kati ya swala mbili ni mtu kuswali swala ya Dhuhr pamoja na swala ya Asr, au swala ya Maghrib pamoja na swala ya Isha, kwa kuswali swala mbili katika wakati wa moja yake, (iwe ni kuunganisha mapema au kuunganisha kwa kuchelewesha), ikiwa kuna udhuru miongoni mwa udhuru zinazoruhusika kisheria kuunganisha swala.

Miongoni mwa udhuru zinazoruhusiwa kuunganisha swala kwa sababu yake, na ambazo hukithiri wakati wa majira ya baridi ni mvua. Na baadhi ya wanazuoni huongeza upepo mkali wa baridi, baridi kali, theluji inayozuia barabara, matope yanayojaa barabarani.

Na kinachomaanishwa na udhuru unaoruhusiwa ili kuunganisha swala ni hali ambazo huwawia watu vigumu kutoka kwenda msikitini kila mara kwa ajili ya swala ya jamaa, kwa hivyo wanaruhusiwa kuunganisha swala. Tofauti na mvua nyepesi ambayo haiwazuii watu kwenda nje kwa ajili ya matembezi au kukidhi mahitaji yao.

Kanuni ya msingi ni kwamba Waislamu kuswali kila swala katika wakati wake maalumu. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: "Na mtakapotulia, basi shikeni Swala kama desturi. Kwani hakika Swala kwa Waumini ni faradhi iliyowekewa nyakati maalumu." [An-Nisaa: 103] Na ndiyo maana hairuhusiki kuunganisha swala isipokuwa ikithibitishwa kuwa kuna udhuru unaoruhusiwa kuunganisha. Na imesimuliwa kutoka kwa Umar bin Khattwab na Ibn Abbas, Mwenyezi Mungu awe radhi nao, na wengineo kwamba kuunganisha swala mbili bila ya udhuru ni mojawapo ya madhambi makubwa zaidi.

Mtu asiyelazimika kuswalia katika jamaa (mkusanyiko) - kama vile mwanamke, mgonjwa - haruhusiwi kuunganisha swala. Kwa sababu hahitaji kuunganisha, bali analazimika kuswali kila swala katika wakati wake. Na vile vile haruhusiwi kuunganisha swala ikiwa udhuru wake utaisha kabla ya kuswali swala ya pili.

Inamtosha Muislamu katika wakati wa kuunganisha swala mbili kuadhini adhana moja, na akimu kwa ajili ya kila Swala. Na pia aswali Sunna zilizowekwa za baada yake, na afanye nyiradi zilizowekwa za baada yake.

Katika misikiti kadhaa, huwa kuna kutofautiana katika kuwepo kwa udhuru unaoruhusu kuunganisha swala. Lakini hukumu ya asili ni kwamba imamu ndiye anayewajibika katika hilo, kwa hivyo anapaswa kujitahidi ikiwa ana elimu na atafute ushauri wa wale walio na elimu. Na ikiwa hatakuwa na dhana kubwa kwamba inaruhusika kuunganisha, basi hataunganisha, itakuwa juu ya watu wa msikiti huo kutobishana.

Majira ya baridi na suala la kuswali usiku, na kufunga saumu

Baadhi ya simulizi zilisema kwamba: "Majira ya baridi ni msimu wa furaha wa muumini; siku yake ilifupishwa kwa hivyo akafunga saumu, na usiku wake ulikuwa mrefu; kwa hivyo akaswali." (Imepokelewa na Al-Bayhaqi katika 'Sunnan Kubra' 8456) Na msimu huu uliitwa hivi kwa sababu mtu anafurahia wakati huo kwa kufanya vitendo mbali mbali vya ibada. Kwa sababu anaweza kufunga saumu wakati wa msimu wa baridi wakati wa mchana bila ugumu wa kuwa na njaa, au kiu kwa sababu ya ufupi wa mchana. Kama vile anaweza kuswali usiku kwa sababu ya urefu wa usiku wake; na anaweza kuunganisha kati ya kuswali na kulala.

Katika baadhi ya simulizi kuna kwamba: "Kufunga saumu wakati wa majira ya baridi ni nyara baridi." (Imepokelewa na Ahmad 18959); Umar, Mwenyezi Mungu awe radhi naye alisema: "Majira ya baridi ni nyara kwa waja." (Imepokelewa na Abu Nu'aim katika Al-Hila 1/51)

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani