Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Janga la ugonjwa ni somo na mawaidha

Katika kutokea magonjwa na majanga kuna masomo mengi na mawaidha ambayo hawatanabahi na kuyatambua isipokuwa wale ambao Mwenyezi Mungu aliangaza ufahamu wake miongoni mwa watu wa imani. Katika somo hili, utajifunza kuhusu baadhi ya masomo haya ambayo yanaongeza imani ya waumini.

  • Kujua masomo na mawaidha yaliyo katika magonjwa ya milipuko yanayofungamanisha mioyo na Mwenyezi Mungu.

Janga la magonjwa ni moja ya majaliwa ya Mwenyezi Mungu yanayoteremka juu ya watu, Waislamu wao na makafiri wao. Lakini hali ya Muislamu anapokuwa katika balaa (janga) si sawa na ile ya wengineo; kwani yeye huamiliana nayo kwa yale ambayo Mola wake Mlezi Mtukufu aliamuru,kama vile kuwa na subira na kufanya sababu za kisheria za kuizuia kabla ya kutokea kwake, na kutafuta tiba baada ya kushikiwa nayo.

"Na wala hawakumheshimu Mwenyezi Mungu kama anavyostahiki kuheshimiwa."

Katika kuenea kwa majanga ya magonjwa kwa sababu ya kiumbe dhaifu ambacho hakiwezi kuonekana isipokuwa kwa kutumia darubini, na yakasababisha hofu na kufadhaika kukubwa katika roho za watu - kama ilivyokuwa katika janga la Corona - kuna ishara inayoonyesha nguvu kubwa za Mwenyezi Mungu Mtukufu, na udhaifu wa viumbe. Hata kama watafikia vipi katika maendeleo na wakamiliki teknolojia ya namna gani, hawawezi kutoka nje ya duara la udhaifu wa kibinadamu. Na pia kuna ishara kwamba Mwenyezi Mungu ana nguvu kubwa madhubuti, ambayo hakuna kitu duniani wala mbinguni kinachoweza kumshinda.

Mipangilio ya Mwenyezi Mungu na kadari yake ni haki

Anachotaka Mwenyezi Mungu, kinakuwa, na asichotaka, hakiwi, ikiwa ni pamoja na misiba na milipuko ya magonjwa. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: "Hautokei msiba katika ardhi wala katika nafsi zenu ila umekwisha andikwa katika Kitabu kabla hatujauumba. Hakika hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi." (Al-Hadid: 22)

Kwa hivyo, Waislamu wanaamini kwamba kila kitu ulimwenguni kilipangwa na Mwenyezi Mungu na akakiandika kabla ya kuumba viumbe. Itikadi hii inawafanya kuwa na utulivu na udhabiti wakati wa hofu. Kwa hivyo wanaipokea mipangilio ya Mwenyezi Mungu kwa vifua vilivyokunjuka.

Kupata mawaidha na kuzingatia:

Mojawapo ya ishara za kuachiliwa mbali na Mwenyezi Mungu wakati wa misiba ni watu kujishughulisha na kuripoti habari bila kuzingatia. Kuzingatia na kupata mawaidha kutokana na kuenea kwa milipuko ya magonjwa na balaa ni desturi iliyoachwa na watu, na ni ibada kubwa. Ilikuja katika kitabu 'Hilyatul-Awliyaa' kutoka kwa Abu Dardaa, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, kuwa alisema: "Kutafakari saa moja ni bora kuliko kusimama usiku katika swala."

Misiba na balaa inayompata Mwislamu ni kwa sababu ya mambo yafuatayo:

١
Kufutiwa mabaya na kunyanyuliwa daraja: Kwa hivyo mja anahitaji kuwa na imani, yakini, uvumilivu na uthabiti katika hali hizi.
٢
Kumbusho: Muislamu anahitaji kuwa macho dhidi ya kughafilika, kupotea na kuwa mbali na Mwenyezi Mungu.
٣
Adhabu: Na hayo yanapotokea, basi lazima mtu atubie, aombe dua kwa unyenyekevu na kuzidisha kumtii Mwenyezi Mungu.

Kumuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu dua kwa unyenyekevu:

Miongoni mwa matendo makuu ya ibada wakati wa misiba hii ni kuwa mja anayemuomba Mwenyezi Mungu dua kwa unyenyekevu, uvunjifu, na kumtii. Pia ni kuwa mja mwenye kuomba kuokolewa na kuondolewa balaa hiyo na Mwenyezi Mungu peke yake. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Kwa nini wasinyenyekee ilipowafika adhabu yetu? Lakini nyoyo zao zilikuwa ngumu, na Shetani akawapambia yale waliyokuwa wakiyafanya." (Al-An 'am 43) Dua ya dhati inamfungulia mtu milango ya mbinguni, na inapenya ndani ya pazia, na inakunja umbali mrefu, na kumleta mja karibu na Mwingi wa rehema. "Na waja wangu watakapokuuliza habari zangu, waambie kuwa Mimi hakika nipo karibu. Ninaitikia maombi ya mwombaji anaponiomba." [Al-Baqara: 186] Wahab bin Munabbih, Mwenyezi Mungu amrehemu, alisema: 'Balaa hushuka ili itoe nje dua.'

Ibn Kathir, Mwenyezi Mungu amrehemu, alisema: "Kwa nini wasinyenyekee ilipowafika adhabu yetu? Na wakaonyesha uhitaji wao juu yetu?" Lakini nyoyo zao zilikuwa ngumu, yaani, hazikulainika wala kunyenyekea. Na Shetani akawapambia waliyokuwa wakiyafanya ya ushirikina na maasia.

"Ni kwa sababu ya vitendo vya mikono yenu."

Mojawapo ya kudanganyika kukubwa zaidi na kufikiri kwamba tuko salama dhidi ya mipango ya Mwenyezi Mungu ni kuamini kwamba tuna kinga dhidi ya misiba hii na milipuko ya magonjwa. Na kwamba jambo la mwisho tunalofikiria ni uwepo wa uhusiano kati ya balaa hizo na dhambi zetu, pamoja na kwamba haya ni katika misingi ya Qur-ani ambayo yamethibiti katika aya zaidi ya moja. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: "Nyinyi, ulipokusibuni msiba ambao nyinyi mmekwisha watia mara mbili mfano wa huo, mnasema: 'Umetoka wapi huu?' Sema: "Huo umetoka kwenu wenyewe." (Al-Imran 165) na alisema: "Na misiba inayokusibuni ni kwa sababu ya vitendo vya mikono yenu. Naye anasamehe mengi." (Ash-Shura: 30)

"Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja wake."

Wakati misiba na balaa zinatokea kwa mfululizo, unadhihirika upole wa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa watu wa imani, kwa kuwapumzisha, kuwalinda kutokana na baa hilo, kuwaepusha na kile kilichotokea wengine wao, na kuwawezesha kuwa na uvumilivu na kuridhia mipangilio ya Mwenyezi Mungu wakati wa shida. Usingekuwa upole wake Yeye aliyetakasika, basi mioyo ingejaa upweke, hofu na mafadhaiko.

As-Saadi, Mwenyezi Mungu amrehemu, anasema katika tafsiri ya aya: "Hakika Mola wangu Mlezi ni Mpole kwa alitakalo." Anamfikishia mja wake wema wake na hisani yake kutokea asipohisi, na kumfikishia kwenye daraja za juu mbali na vitu anavyovichukia."

Kutegemea Mwenyezi Mungu Mwenye Nguvu, Mtukufu:

Kuwa na imani na Mwenyezi Mungu na kumtegemea ni mojawapo ya njia kuu za kushinda majaribio na balaa. Kwa hivyo mtu anapaswa kuwa na yakini kwamba faraja iko karibu. Pia eneza matumaini katika wale walio karibu nawe na uepukane na kuwa na wasiwasi na kutokuwa na matumaini; kwa maana ugumu mmoja hauwezi kushinda wepesi mbili: "Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi. Hakika pamoja na uzito upo wepesi." (Ash-Sharh: 5, 6)

"Enyi mlioamini! Chukueni hadhari yenu! Na mtoke kwa vikosi au tokeni nyote pamoja!"

Miongoni mwa desturi za Mwenyezi Mungu alizoweka ulimwenguni ni kwamba; kufanya sababu za kisheria zinazowezekana, kuwa ni mojawapo ya sababu za kuzuia maovu. Na hivyo ndivyo walivyofanya Mitume na watu wema. Na hilo ni katika kumtegemea Mwenyezi Mungu kikamilifu, na kufikia kuwa mja wake sawasawa.

Uhakika wa kumtegemea Mwenyezi Mungu ni moyo kumtegemea Mwenyezi Mungu pamoja na kufanya visababishi vya mambo. Kwani kumtegemea Mwenyezi Mungu na kuacha kufanya visababishi ni kutoa dosari katika sheria na kuwa na upungufu wa kiakili. Na pia kufanya visababishi peke yake bila ya moyo kumtegemea Mwenyezi Mungu ni upungufu katika kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kufanya ushirikina katika visababishi hivyo.

"Hakika haya maisha ya dunia ni starehe ipitayo tu."

Kiumbe kilichofichikana ambacho kimewanyima watu wa duaniani furaha yao, raha zao, usalama wao, utulivu wao na maisha yao ya kawaida. Basi, je, nafaa kwa mtu mwenye akili timamu, achilia mbali Muumini, kuichukua dunia hii kama mahali pa kutua, pa kuipigania na pa kushindana juu ya mambo yake yasiyo na thamani?

"Bali niogopeni Mimi mkiwa nyinyi ni Waumini."

Hakuna shaka kwamba virusi hivi ni miongoni mwa ishara za Mwenyezi Mungu za kimaumbile ya kiulimwengu, ambazo kwazo Mwenyezi Mungu huwahofisha waja wake, na anawasukuma kwazo ili kuwapa mawaidha na waweze kuzingatia, na kufufua uja wa kumhofu. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: "Nasi hatutumi Ishara ila kwa ajili ya kuhofisha." (Al-Israa: 59)

Kuhuisha uja wa mtu kuwa na hofu ni katika ishara za Mwenyezi Mungu:

Ilikuwa ni katika mwongozo wa Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kuhofu ishara za Mwenyezi Mungu. Imesimuliwa kutoka kwa Anas,Mwenyezi Mungu amridhie, kuwa alisema: Zilikuwa pepo kali zinapovuma, wasiwasi ilikuwa inaonekana kwenye uso wa Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake (kwa kuhofu kwamba upepo huo huenda ni ishara ya ghadhabu ya Mwenyezi Mungu). (Al-Bukhari 1034)

"Na ukipata faragha, fanya juhudi."

Muda ndio mtaji mkuu wa Muislamu katika dunia hii, nao ndio mali yenye thamani kubwa zaidi kuliko thamani nyingine ile. Ibn Abbas, Mwenyezi Mungu amridhie, alisimulia kutoka kwa Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kwamba alisema: "Kuna neema mbili ambazo watu wengi hupunjika ndani yake; Afya njema na wakati wa mapumziko." (Al-Bukhari 6412)

Mtu mwenye hekima daima huchukua fursa katika wakati wake. Na hilo linazidi katika wakati wa shida na majaribio; kwa hivyo hutumia wakati wake vyema katika kila kitu kinachomleta karibu na Mwenyezi Mungu. Ibn al-Qayyim, Mwenyezi Mungu amrehemu, anasema: "Kupoteza wakati ni jambo kubwa zaidi kuliko kufa; kwa sababu kupoteza wakati hukukata wewe mwenyewe mbali na Mwenyezi Mungu na Akhera, na kifo hukukata mbali na dunia tu na watu wake."

Al-Shanqiti, Mwenyezi Mungu amrehemu, anasema kuhusu maneno ya Mwenyezi Mungu: "Na ukipata faragha, fanya juhudi. Hii ni suluhisho ya tatizo la mtu kutokua na cha kufanya, jambo ambalo limeushughulisha sana ulimwengu. Kwani Muislamu hakuwachiwa utupu katika wakati wake; kwa sababu ima yuko katika kazi ya kidunia, au katika kazi ya Akhera."

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani