Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Kamari na Maysir

Somo hili linafafanua maana ya kamari na maysir, na linabainisha hukumu zake na madhara yake kwa mtu binafsi na jamii.

  • Kujifunza kuhusu maana ya kamari na maysir.
  • Kujua hukumu ya kamari katika sheria ya Kiislamu.
  • Kubainisha aina za maysir na madhara yake.

Kamari au maysir ni nini?

Kamari ni kila mchezo ambao upande mmoja au zaidi unapata faida na mwingine unapata hasara. Kwa hivyo kila mshiriki huwa kati ya kupata faida (mali au mengineyo), au kupata hasara ya mali hiyo au mengineyo.

Hukumu ya Kamari

Kamari imeharamishwa kwa Kitabu (Qur-ani), Sunna na maafikiano ya wanazuoni.

Mshindi katika kamari na maysir hupata faida, lakini Mwenyezi Mungu, Mwenye Nguvu, Mtukufu alibainisha kwamba dhambi zake na madhara yake ni makubwa kuliko faida zake na manufaa yake. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu, "Wanakuuliza juu ya mvinyo na kamari. Sema: Katika hivyo, zipo dhambi kubwa na manufaa kwa watu. Lakini dhambi zake ni kubwa zaidi kuliko manufaa yake." (Al-Baqarah: 219)

Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu, "Enyi mlioamini! Bila ya shaka mvinyo, na kamari, na masanamu, na kupiga ramli, ni uchafu katika matendo ya Shetani. Basi jiepusheni navyo, ili mfaulu." (Al- Maaidah: 90)

Madhara ya kamari na maysir kwa mtu binafsi na jamii:

١
Kuleta uadui na chuki kati ya watu. Kwa maana mmoja wa wawachezaji au washindani anapochukua mali za mtu mwingine kwa kucheza tu, basi hilo hujaza vifua vyao chuki dhidi yake, na linawafanya kungojea fursa ya kumdhuru pia. Huu ndio uhakika na hali halisi ambayo hata jamii inaijua, ambayo inaoyesha ukweli wa kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, "Hakika Shetani anataka kutia kati yenu uadui na chuki kwa mvinyo na kamari." [Al-Maidah: 91]
٢
Kumzuia mtu kumdhukuru Mwenyezi Mungu na kuswali. Haya ni makusudio makubwa zaidi miongoni mwa makusudio ya Shetani. Kama ilivyoelezwa katika aya ya mwisho ya surat Al- Maaidah iliyotangulia, "Na awazuieni kumkumbuka Mwenyezi Mungu na kuswali."
٣
Kupoteza mali na kuharibu raslimali. Je, ni matajiri wangapi wamekuwa mafukara kwa sababu ya kamari?
٤
Kuwa na uraibu wa michezo na kamari: Kwa maana mshindi anakuwa na hamu na tamaa ya kuzidisha faida kutokana na kucheza kamari. Naye aliyeshindwa anaendelea kucheza akitumai kurejesha kile alichopoteza.
٥
Kuvunjika kwa familia: Uraibu wa kamari husababisha mtu anayecheza kamari kupuuza mambo ya familia yake, na kupoteza mali husababisha matatizo ya kifedha na kisaikolojia, ambayo mara nyingi huishia katika talaka na kuvunjwa kwa familia.

Aina za Maysir (bahati nasibu):

1. Kila mchezo ambao mshindi huchukua kitu kutoka kwa mshindwa: kama vile kikundi cha watu wanaocheza kadi, na kila mmoja wao akaweka kiasi fulani cha mali, kwa hivyo yeyote atakayeshinda, anachukua mali hizo zote.

2- Kuweka rahani kwamba timu fulani au mchezaji fulani au mfano wa hivyo atashinda: Kwa hivyo, ikiwa timu yake itashinda, anashinda mali hizo. Na ikiwa timu yake itashindwa, basi anapoteza mali hizo.

3- Bahati nasibu na kadi za bahati nzuri: Hili ni kama vile kununua kadi kwa Dola kwa hivyo akawa amepata kuingia katika mchezo wa kuchukua kadi ya bahati nzuri. Kadi yake ikishinda, anapata zaidi ya thamani yake, sawa kiwe kichache alichopata au kingi.

4- Kushiriki katika mashindano kwa simu au kwa ujumbe wa rununu ambao umewekewa zaidi ya gharama zake za kawaida. Vile vile michezo yote inayofanywa kwa viungo vya mwili kama vile kukimbia, au michezo ya umeme na ya kielektroniki, au kupitia tovuti za mtandaoni, ambayo mchezaji huwa kati ya uwezekano mwili: kushinda mali au kuipoteza.

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani