Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Mkopo

Katika somo hili, tutajifunza kuhusu maana ya mkopo, na baadhi ya hukumu zake katika sheria ya Kiislamu.

  • Kujua maana ya mkopo, hukumu yake na masharti ya kuwa kwake sahihi.
  • Kujua hali za mdaiwa wakati wa kulipa deni.

Mwenyezi Mungu Mwenye Nguvu Mtukufu aligawanya riziki kati ya watu kwa uadilifu na hekima yake. Basi kati yao kuna matajiri na maskini, wenye uwezo na wahitaji. Na desturi ya watu ikawa kwamba baadhi yao wanakopa kutoka kwa wengine cha kuwasaidia kutimiza mahitaji yao. Na kwa sababu sheria ya Mwenyezi Mungu, Mwenye Nguvu, Mtukufu ni kamilifu na pana, ilikuja na hukumu kadhaa zinazohusiana na mikopo. Mwenyezi Mungu Mtukufu amebainisha mkopo katika aya ndefu zaidi katika Qur-ani Tukufu, ambayo ni aya ya 282 ya Suratul-Baqara, nayo inaitwa Aya ya deni.

Maana ya mkopo

Ni kupeana mali kwa njia ya kusaidia anayetaka kunufaika nayo, kisha arudishe badili yake.

Hukumu ya mkopo

Mkopo ni jambo linalopendekezwa, na linaloruhusiwa kwa mkopaji. Na kukopa siyo katika kuomba kunakochukiwa, kwa sababu mkopaji huchukua mali ili afaidike nayo katika kukidhi mahitaji yake, kisha arudishe badili yake.

Lakini ikiwa mkopo unaleta faida kwa mkopeshaji, basi hiyo ni riba iliyoharamishwa, kama vile kumkopesha pesa ili azirudishe na kitu zaidi juu yake. Na vile vile, ikiwa mkataba mwingine, kama vile uuzaji na mwingineo, utajumuishwa katika mkopo, basi hilo ni haramu, kwani mkopo hauruhusiwi kuunganishwa na kuuza au kununua.

Hekima ya kuhalalishwa mkopo

Uislamu uliruhusu mkopo kwa sababu ya uzuri ulio ndani yake kwa watu, na kuwaepesishia mambo yao, na kuondoa shida zao, na kuwafariji wahitaji. Na huu ni mojawapo ya milango ambayo humleta mkopeshaji karibu na Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kwa kiasi hitaji lilivyokuwa kubwa, ndivyo thawabu zinazidi kuwa kubwa.

Inapendekezwa kuuandika mkopo, uwe mdogo au mkubwa, kwa kuuwekea mashahidi. Uandikwe kiasi chake, aina yake, na muda wake ili kuuhifadhi mkopo huo, na ili kumhakikishia mkopeshaji kwamba haki yake haitapotea ima kwa kifo cha mkopaji, kusahau kwake, au kukataa kwake, na mfano wa hayo. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema katika Aya ya deni, "Enyi mlioamini! Mnapokopeshana deni kwa muda uliowekwa, basi liandikeni. Na mwandishi aandike baina yenu kwa uadilifu, wala mwandishi huyo asikatae kuandika kama alivyomfunza Mwenyezi Mungu. Basi na aandike, na mwenye deni juu yake aandikishe, naye amche Mwenyezi Mungu, Mola wake Mlezi. Wala asipunguze chochote ndani yake." [Al-Baqarah: 282] Na akasema katika aya hiyo hiyo, "Wala msipuuze kuliandika deni likiwa dogo au kubwa mpaka muda wake. Hayo ndiyo haki zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu, na ndiyo sawa zaidi kwa ushahidi, na vyema zaidi ili msiwe na shaka." [Al-Baqarah: 282]

Masharti ya kuufanya mkopo kuwa sahihi

١
Kwamba mkopo utimie kwa njia ya ofa na kukubali, au chenye kusiamama mahali pa viwili hivyo.
٢
Kwamba mwana mkataba huo - mkopeshaji au mkopaji - lazima awe mtu mzima, mwenye akili timamu, mwenye busara, ana chaguo, ana uwezo wa kutoa msaada na kupokea kitu.
٣
Kwamba mali hiyo ya mkopo iwe inaruhusika katika sheria.
٤
Kwamba mali hiyo ya mkopo iwe inajulikana kiasi chake.

Ni lazima kwa mwenye kukopa mali kutoka kwa wengine aazimie kuitekeleza. Kwa hivyo ni haramu kwa mtu kuchukua mali za watu ilhali hakusudii kuwarudisha mali hizo. Na wakati wa kulipa deni unapofika, inamlazimu kulilipa. Imesimuliwa kutoka kwa Abu Huraira - Mwenyezi Mungu - kwamba Mtume - rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - alisema, "Mwenye kuchukua mali za watu akitaka kuzilipa, basi Mwenyezi Mungu atamlipia hizo. Na mwenye kuzichukua huku anataka kuziharibu, basi Mwenyezi Mungu atamharibu." (Al-Bukhari 2387)

Hali mbalimbali za wadaiwa wakati wa kulipa deni

١
Yule ambaye hana kitu kabisa. Basi huyu ni lazima kumpa muhula kwa sababu ya ugumu alio nao. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema, "Na akiwa (mdaiwa) ana shida, basi (mdai) angoje mpaka afarijike. Na mkilifanya deni kuwa ni sadaka, basi ni bora kwenu, ikiwa mnajua." [Al-Baqarah: 280]
٢
Yule ambaye mali yake ni mengi zaidi ya deni lake. Huyu inamlazimu kulipa deni lake, kwani ni haramu kwa mwenye deni tajiri kuchelewesha malipo ya deni kupita wakati wake unapofika. Imesimuliwa kutoka kwa Abu Huraira - Mwenyezi Mungu amridhie - kwamba, Mtume wa Mwenyezi Mungu - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie - alisema, "Mtu tajiri kuchelewesha kulipa deni ni dhuluma." (Bukhari 2288, Muslim 1564)
٣
Yule ambaye mali yake ni sawa na deni lake. Huyu inamlazimu kulipa deni lake hilo.
٤
Yule ambaye mali yake ni kidogo kuliko deni lake. Huyu amefilisika, na anazuiliwa ikiwa wadaiwa au baadhi yao watamdai, na mali yake itagawanywa kati yao kulingana na deni lake kwa kila mmoja wao.

Hukumu ya kuweka mali katika benki

١
Kuweka pesa katika mabenki ya Kiislamu ambayo yanashughulika kwa mujibu wa masharti ya Sharia inaruhusiwa.
٢
Ama kuweka mali katika benki zenye riba, hilo halitoki katika hali mbili. Ya kwanza ni kuwe kuweka huko anataka kulipwa riba juu yake. Hili ni riba iliyoharamishwa, na kuweka huku hakuruhusiki. Na hali ya pili ni kuweka katika akaunti ya sasa isiyokuwa na riba. Na hii pia hairuhusiki kwa sababu ndani yake kuna kuisadia benki kutumia mali (pesa) katika shughuli zake zenye riba. Na inaondolewa katika hukumu hii hali ya dharura halisi, kama vile mwekaji ahofie mali (pesa) yake kupotea au kuibiwa, wala hakupata njia mbadala halali ya kuhifadhi mali (pesa) zake hizo. Hapo, inaruhusika kuweka hapo mali yake kwa sababu ya dharura hii.

Hairuhusiki kumuwekea sharti mdaiwa kulipa faini ikiwa atachelewa kulipa deni kwa wakati uliowekwa, kwa sababu hiyo ni riba. Na hairuhusiki kukopa ikiwa kuna sharti hili, hata kama mkopaji anafikiria kuwa ataweza kulipa kwa wakati bila kuwepo kwa faini hii, kwa sababu huko ni kuingia katika mkataba ambao atalazimika kulipa riba.

Kufanya wema wakati wa kulipa mkopo

Kufanya wema wakati wa kulipa mkopo - kama vile akimkopesha kitu kisha yeye arudishe kilicho bora kuliko hicho, au kikubwa kuliko hicho, au kingi kuliko hicho. Hili linapendekezwa ikiwa siyo sharti. Kwa sababu hili ni katika kulipa kwa uzuri, na maadili ya ukarimu. Lakini ikiwa ni sharti, basi ni riba iliyoharamishwa.

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani