Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Uhakika wa Zaka na malengo yake

Zaka ndiyo nguzo ya tatu ya Uislamu. Katika somo hili, utajifunza kuhusu uhakika wa Zaka, malango yake, na hekima katika kuiweka katika sheria.

  • Kujua uhakika wa Zaka.
  • Kujua malengo ya kuiweka katika sheria.
  • Kujua makundi ya wale wanaostahili kupewa Zaka.

Zaka

Zaka ndiyo nguzo ya tatu ya Uislamu. Nayo ni wajibu wa kimali ambao Mwenyezi Mungu aliufaradhisha juu ya matajiri kuwapa masikini, wahitaji na watu wengineo wanaostahili sehemu maalumu katika mali zao ili kuondoa shida zao.

Malengo ya Zaka

1. Kupenda mali ni silika ya kibinadamu ambayo humfanya mwanadamu awe na hamu kubwa ya kuihifadhi na kuishika. Kwa hivyo, Sheria iliwajibisha kutoa Zaka ili kuisafisha nafsi kutokana na uovu wa ubahili na uchoyo, na kutibu kuipenda dunia na kushikamana na vitu vyake visivyo na thamani. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema, "Chukua sadaka katika mali zao, uwasafishe na uwatakase kwazo." (Tawba: 103)

2. Kutoa Zaka kunafanikisha suala la kushikamana na kuungana. Kwa sababu, nafsi ya mwanadamu imefanywa kuwapenda wanaoifanyia uzuri. Kwa hilo, wanajamii wa Kiislamu wataishi pamoja kwa kupendana na kushikamana, kama jengo lililokamatana, linaloimarishana lenyewe kwa lenyewe, na yatapungua matukio ya wizi, uporaji, na utapeli.

3. Inatimia maana ya uja na unyenyekevu mkamilifu, na kujisalimisha kamili kwa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote. Tajiri anapotoa Zaka ya mali yake, anakuwa anatekeleza sheria ya Mwenyezi Mungu na kutimiza amri yake. Na pia katika kuitoa kuna kumshukuru yule aliyeneemesha kwa neema hiyo, na Mwenyezi Mungu atamlipa kwa shukrani hii. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema, "Mkishukuru, nitawazidishia." (Ibrahim: 7)

4. Kwa kuitoa, linafikiwa lengo la dhamana ya kijamii na uwiano wa kijamii kwa kiwango fulani kati ya vikundi vya jamii. Kwa maana, kuitoa na kuwapa wastahiki wake hakuachi rasilimali kurundikana mikononi mwa vikundi fulani tu wakawa wanaihodhi wao tu. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema, "Ili yasiwe yakizunguka baina ya matajiri tu miongoni mwenu." (Al-Hashr: 7)

Zaka anapewa nani?

Uislamu umeshafafanua wale wanaostahiki Zaka. Mwislamu anaruhusiwa kukipa kikundi kimoja kati ya wapokezi wa Zaka au azipe taasisi na mashirika ya kihisani ambayo yanazigawanya kwa wapokezi wake miongoni mwa Waislamu, ingawa ni bora zaidi kuigawanya katika nchi anayoishi aliyeitoa Zaka hiyo.

Wapokezi wa Zaka

١
Fukara: Naye ni yule ambaye hawezi kupata chochote kabisa, au anaweza kupata chini ya nusu ya kile kinachomtosha kwa muda wa mwaka mmoja.
٢
Maskini: Ni yule anayepata nusu ya kinachomtosha au kingi kwa muda wa mwaka mmoja.
٣
Wanaozishughulikia: Ni wale wafanyakazi walioajiriwa na wakusanyaji wake, ambao Imamu huwatumia katika kukusanya na kugawanya Zaka.
٤
Wa kutiwa nguvu nyoyo zao: Nao ni mabwana wanaotiiwa katika kaumu zao, ambao wanatarajiwa kusilimu au kunatarajiwa kusilimu kwa wenzao wa mfano wao, au kutia nguvu imani yao, au kuwazuilia kuwadhuru Waislamu, au wale wanaohofiwa uovu wao.
٥
Kukomboa watumwa: Hawa ni watumwa wenye mikataba kati yao na mabwana wao kwamba walipe mali ili wawe huru. Kwa hivyo, inaruhusiwa kumnunua mtumwa kwa mali ya Zaka, au kuwakomboa mateka wa Kiislamu.
٦
Wenye madeni: Ni wale ambao walikopa kwa ajili yao wenyewe - mradi tu ilikuwa kwa ajili ya jambo linaloruhusiwa - kisha wakashindwa kulipa, au ambao walikopa kwa ajili ya kurekebisha uhusiano kati ya watu.
٧
Katika njia ya Mwenyezi Mungu: Hawa ni wapiganaji vita wanaopigana kwa jihadi kwa hiari ili kuutetea Uislamu, wala hawana fidia wala mshahara katika mali ya Waislamu.
٨
Wasafiri: Ni msafiri ambaye amekatikiwa njia katika mji wa kigeni. Atapewa cha kumfikisha anakokwenda, mradi tu safari yake isiwe ya haramu.

Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema akibainisha wapokezi wa Zaka, "Wa kupewa sadaka ni mafukara, na masikini, na wanaozitumikia, na wa kutiwa nguvu nyoyo zao, na katika kukomboa watumwa, na wenye madeni, na katika njia ya Mwenyezi Mungu, na wasafiri." (Tauba: 60)

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani