Endelea kujifunza

Umeshaingia
Jisajili sasa kwenye jukwaa la Taa ili uanze kujifunza, na fuatialia maendeleo yako, na kukusanya pointi, na uingie kwenye mashindano.Baada ya kujisajili, utapata cheti cha kielektroniki katika mada ambazo utajifunza.

Sehemu ya sasa:

Somo Zawadi

Katika somo hili, tutajifunza kuhusu maana ya zawadi, na baadhi ya hukumu zinazohusiana nayo.

  • Kujua maana ya zawadi na hekima iliyo ndani yake.
  • Kujua hukumu za kisheria zinazohusiana na zawadi.
  • Kuhimiza kutoa zawadi kwa ajili ya kutafuta malipo kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye, Nguvu, Mtukufu.

Hakika Mwenyezi Mungu, Mwenye Nguvu Mtukufu, ni mkarimu na anapenda kutoa kwa wingi na ukarimu. Na Mtume wa Mwenyezi Mungu, alikuwa mkarimu wa watu wote, na alikuwa akikubali zawadi na analipa juu yake, na anaitia kuikubali, na anahimiza juu yake. Na kutoa kulikuwa katika mambo yanayopendeza zaidi kwake, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie.

Ufafanuzi wa zawadi

Ni kummilikisha mtu kitu papo hapo bila malipo.

Na kauli yetu: "Kumilikisha" inaashiria kwamba mkataba wa zawadi ni katika mikataba ya kumilikisha.

Na maana ya "kitu" ni kitu chochote. Na vinaingia ndani yake vitu kama vile mali na visivyokuwa mali.

Na neno "kumilikisha kitu" liliondoa "kutoa zawadi ya manufaa" kwa sababu mbili:

١
Ya kwanza ni kwamba manufaa hayaitwi mali kulingana na baadhi ya wanazuoni wa kisheria.
٢
Ya pili ni kwamba kutoa zawadi ya manufaa kunaitwa vingine kulingana na wanazuoni wa kisheria, yaani "Al-'ariyya (kuazima)."

Pia kitu kingine kilichotoka kwa kuali "kumilikisha" ni kumuondolea mtu deni, hata ikiwa ni kwa lafudhi ya zawadi. Kwa sababu kumuondolea mtu deni kunazingatiwa kwamba ni kuliangusha.

Hiba pia huitwa hadiyya (zawadi) au 'Atwiyya (kipawa) na hayo yote yanaingia katika mlango wa kufanya wema, hisani, kuunga uhusiano na kufanya mazuri.

Hukumu ya kutoa zawadi

Kutoa zawadi kunapendekezwa kwa sababu ya yale yaliyo ndani yake ya kuunga mioyo, kupata thawabu na kuleta upendo. Kitabu Kitakatifu, Sunna tukufu, makubaliano ya wanazuoni viliashiria kupendekezwa kwa jambo la kutoa zawadi.

Sheria ilihimiza kutoa zawadi kwa sababu ndani yake kuna kusafisha nafsi kutokana na uchafu wa ubahili, uchoyo, tamaa, na kwa sababu ya yale yaliyo ndani yake ya kuunga mioyo, kuimarisha msingi wa upendo kati ya watu, haswa ikiwa ni kwa jamaa wa mtu, jirani au adui. Ugomvi unaweza kutokea, na kujitenga na kupeana mgongo, na ukakatwa uhusiano wa jamaa, kisha zawadi ikaja na ikasafisha mioyo na kuondoa kila kitu kinachosababisha mgawanyiko kati ya watu. Mwenye kutoa kitu kama zawadi kwa ajili ya kuutafuta uso wa Mwenyezi Mungu Mtukufu, atapata malipo na thawabu.

Imesimuliwa kutoka kwa 'Aaisha - Mwenyezi Mungu awe radhi naye - kuwa alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, - alikuwa akipokea zawadi na akilipa juu yake. (Al-Bukhari, 2585)

Imesimuliwa kutoka kwa Ibn Abbas - Mwenyezi Mungu awe radhi naye - kuwa alisema, "Mtume wa Mwenyezi Mungu - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie - alikuwa mkarimu zaidi wa watu wote. Na alikuwa mkarimu zaidi katika Ramadhani wakati Jibril anapokutana naye. Na alikutana naye kila usiku wa Ramadhani, na anamsomesha Qur-ani. Kwa hivyo, Mtume wa Allah - rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie - anakuwa mkarimu zaidi wa heri hata kuliko upepo ulioachiliwa." (Al-Bukhari 6, na Muslim 2308)

Nguzo za zawadi

Wanazuoni walikubaliana kwamba kuwasilisha (ofa) ni mojawapo ya nguzo za zawadi, na wakatofautiana katika mengineyo. Kwa hivyo, zawadi inatimia kwa kuiwasilisha tu, (na hilo ni kufanyika kwa chochote kinachoashiria kwamba mtoaji zawadi ametoa zawadi), lakini huyo aliyepewa hawezi kumiliki alichopewa kama zawadi isipokuwa kwa kuikubali na kuipokea. Kwa hivyo kuikubali na kuipokea ni ili athari zake zitokee, na siyo kwa ajili ya kuusimamisha mkataba huu.

Masharti ya zawadi

١
Awe mtoa zawadi miongoni mwa wanaoweza kusaidia.
٢
Awe mtoa zawadi ni mmiliki wake au aliyeidhinishwa kusaidia.
٣
Awe mtoa zawadi ameridhia. Kwani aliyelazimishwa hajukumishwi mkataba wowote.
٤
Ni sharti katika aliyepewa zawadi kwamba awe ana uwezo wa kumiliki. Kwa hivyo haiwi sahihi kumpa zawadi mtu ambaye haruhusiwi kumiliki. Na uwezo huo unakuwa ikiwa mtu huyo ni katika wale waliojukumishwa na sheria. Ama yule ambaye hakujukumishwa na sheria, atakubaliwa zawadi hiyo na mlezi wake.
٥
Kuwepo anayepewa zawadi. Kwa maana, zawadi ni kumilikisha. Na haiwezekani kumilikisha asiyekuwepo.
٦
Anayepewa zawadi anafaa awe mahususi. Kwa hivyo, ikiwa aliyepewa zawadi si mahususi, kama vile mtoa zawadi akisema: Nimempa zawadi ya nyumba yangu fulani au kaka yake. Basi kuna hilafu kati ya wanazuoni kuhusu usahihi wake.
٧
Iwe ni kupeana zawadi ya kitu kinachoruhusika kunufaika nacho. Na hata kama hairuhusiki kukiuza, masuala ya zawadi ni pana zaidi kuliko masuala ya mabadilishano.
٨
Kiwe kilichotolewa kama zawadi kinapatikana. Na kuendesha kitu kisichokuwapo kunategemea kuwepo kwake. Ni sahihi kupeana zawadi ya kitu kisichojulikana, na kisichokuwepo ikiwa kinatarajiwa kuwepo.

Wanazuoni walitofautiana kuhusiana na sharti la kwamba ni lazima zawadi iwe inajulikana. Na pia katika sharti la kwamba ni lazima iwe imegawanywa, na siyo imejumuishwa na kuenea katika vitu vingine.

Hukumu ya kutoa zawadi ili kupata masilahi fulani

Mwenye kumpa zawadi afisa msimamizi, au mfanyakazi, au wengineo kwa ajili ya kupata masilahi fulani ambayo hana haki nayo, basi hilo linakuwa haramu kwa mtoa zawadi na anayepewa zawadi. Kwa sababu hiyo ni rushwa ambayo amelaaniwa mwenye kuichukua na mwenye kuitoa.

Ikiwa ataitoa kama zawadi ili kujizuilia udhalimu fulani, au ili apewe haki yake ya wajibu, basi zawadi hii ni haramu kwa anayeikuchukua, lakini inaruhusiwa kwa mtoaji ili kuhifadhi haki yake na kuuzuia uovu wa huyo anayeichukua.

Imesimuliwa na Abu Humaid As-Saidi, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, kuwa alisema: Nabii, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alimtumia mwanamume fulani kutoka kwa Banu Asad, aitwaye Ibnul Utbiyyah, kwa ajili ya kukusanya sadaka. Aliporudi, akasema: Hii ni yenu, na hii yangu, nimepewa kama zawadi. Kwa hivyo, Nabii rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake akasimama juu ya mimbari, akamhimidi na kumsifu Mwenyezi Mungu, kisha akasema, "Ana nini mfanyakazi tunayemtuma, kisha anakuja na kusema, 'Hii ni yako, na hii ni yangu. Kwa nini hakukaa katika nyumba ya baba yake na mama yake, kisha akaona kama atapewa zawadi au la. Ninaapa kwa yule ambaye nafsi yangu iko mikononi mwake, hatachukua chochote kwayo isipokuwa atakuja nayo Siku ya Qiyama akiibeba shingoni kwake. Ikiwa ni ngamia, atakuwa analia kwa sauti ya ngamia, au ng'ombe akilia kwa sauti ya ng'ombe, au kondoo kwa sauti ya kondoo." Kisha akainua mikono yake hadi tukaona weupe wa kwapa zake. "Je, nimefikisha?" mara tatu. (Al-Bukhari 7174, na Muslim 1832) Khuwaar ni sauti ya ng'ombe. Rugha ni sauti ya ngamia. Ghura ni weupe uliochanganyika na kahawia. Ta'iar ni kulia kwa sauti kubwa sana.

Umemaliza somo kwa ufanisi


Anza mtihani